Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Samia ateua mrithi wa DPP Biswalo
Habari Mchanganyiko

Samia ateua mrithi wa DPP Biswalo

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemteua Sylvester Mwakitalu kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kabla ya uteuzi huu, Mwakitalu, alikuwa Mkurugenzi wa Huduma za Taasisi, katika Ofisi ya Msajili wa Hazina, anachukua nafasi ya iliyoachwa wazi na Biswalo Mganga ambaye tarehe 11 Mei 2021, aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Pia, Rais Samia amemteua Joseph Pande kuwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka (DDPP). Pande anachukua nafasi ya Edson Athanas Makallo ambaye atapangiwa majukumu mengine.

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Mashtaka Tanzania (DPP), Biswalo Mganga

Uteuzi huu, umetangazwa leo Jumamosi, tarehe 15 Mei 2021 na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu.

Msigwa amesema, wateuliwa hao, wataapishwa Jumanne, tarehe 18 Mei, 2021 kuanzia saa 9:00 alasiri, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!