Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Samia akemea ‘vita’ ya uwekezaji
Habari za Siasa

Samia akemea ‘vita’ ya uwekezaji

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan amekemea vita baina ya wawekezaji hasa wanaozalisha bidhaa zinazofanana. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza kabla ya kuzindua maonesho ya bidhaa zinazozalishwa na viwanda vilivyomo Mkoa wa Pwani leo tarehe 29 Oktoba 2018, Samia amesema, hakuna haja ya wawekezaji kupigana vita wenyewe kwa wenyewe bali watafute njia ya kuboresha bidhaa zao ili zipate soko.

Samia amesema, katika Mkoa wa Pwani kuna changamoto ya wawekezaji kupigana vita, ambapo ameutaka uongozi wa mkoa huo kukaa na wawekezaji ili kuondoa changamoto hiyo.

“Changamoto ni kupigana vita wawekezaji kwa wawekezaji, hasa wa bidhaa zinazofanana, uongozi wa mkoa uangalie hilo, hakuna haja wawekezaji kwa wawekezaji kupigana vita, mkuu wa mkoa hilo nakuachia wewe kwa sababu unajua uwekezaji wako,” amesema.

Katika hatua nyingine, Samia amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Everist Ndikilo kuingia makubaliano na wawekezaji wanaotumia malighafi zinazochimbwa, ili wapande miti katika mashino wanayochimba, kuepuka maeneo kuwa jangwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

error: Content is protected !!