Tuesday , 26 September 2023
Home Kitengo Michezo Samia aipongeza klabu ya Yanga kwa hatua iliyofikia
Michezo

Samia aipongeza klabu ya Yanga kwa hatua iliyofikia

Spread the love
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, ameipongeza klabu ya soka ya Yanga, kwa hatua waliyofikia katika michuano ya shirikisho – CAF Confederation CUP. Anaandika Mwandishi Wetu…(endelea).

Katika ujumbe wake, kupitia ukurasa wake wa twitter, Rais Samia amesema, klabu ya Yanga ya jijini Dar es Salaam, imeandika historia na imelipa hadhi kubwa taifa lake.

“Hongereni sana Yanga kwa hitimisho la mchezo wa fainali. Historia mliyoandika katika safari yenu ya michuano hii ni kubwa na ya heshima kwa taifa letu. Nawatakia kheri katika mipango yenu katika siku zijazo,” ameeleza.

Yanga iliyokuwa inashiriki michuano hiyo, imekuwa timu ya kwanza katika kipindi cha miongo mitatu iliyopita, kufika fainali ya michuano ya CAF.

Katika mchezo wake wa jana wa fainali dhidi ya USM Alger, klabu hiyo ya mitaa ya Twiga na Jangwani, ilishinda kwa goli moja lililofungwa kwa njia ya penati na Djuma Shaban.

Ndoto za Yanga kutwaa Kombe la Shirikisho zimefifishwa na mabao ya ugenini licha ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 katika fainali ya pili dhidi ya USM Alger.

Yanga waliandika historia yao mpya tangu kuanzishwa kwake mwaka 1935 kufikia hatua hiyo na kwa kushinda ugenini, katika mechi ya marudiano ya fainali ya kombe hilo.

Yanga imekosa taji la kwanza la CAF kutokana na faida ya bao la ugenini kuwabeba Waalgeria.

Wenyeji ilitwaa taji hilo la kwanza kwao baada ya awali kushinda ugenini 2-1 na matokeo ya jumla kuwa sare ya 2-2, lakini kanuni ya bao la ugenini ikawapata taji hilo kwenye mchezo huo uliochezwa Uwanja wa 5 Jullieti 1962 mjini Algers.

Yanga walionyesha kiwango kikubwa cha mchezo ugenini tofauti na ilivyocheza jijini Dar.

Kocha Nasreddine Nabi aliwatumia mabeki watano, ikiwamo Dickson Job kama kiungo namba sita na kuwabana wenyeji na kufanikiwa kupata bao hilo pekee dakika ya saba tu likiwekwa kimiyani kwa penalti na beki Djuma Shaban baada ya Kennedy Musonda kuchezwa madhambi.

Kanuni za CAF zinaeleza, pale matokeo yanapolingana, huangalia timu ipi iliyoshinda magoli mengj ugenini; kanuni ambayo imedumu kwa miaka mingi sana duniani.

Hata hivyo, katika siku za karibuni, hasa kwenye michuano ya UEFA, kanuni hii imefutwa na hivyo, kama ingekuwa UEFA, mechi ya jana ingeongezwa dakika 30 au ingekwenda penalti moja kwa moja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMichezo

Piga pesa kupitia Derby ya London Kaskazini kwa kubadhiri na Meridianbet

Spread the love NAJUA umesikia na unazijua Derby nyingi kutoka jiji la London,...

BiasharaMichezo

Wikiendi hii ushindi upo Meridianbet na si kwingine

Spread the love USHINDI huu ni wako mteja wa Meridianbet kama mechi...

BiasharaMichezo

Safari ya Gavi kutoka Academy ya Real Betis mpaka Barca

Spread the love  ANITWA Pablo Martín Páez Gavira ‘Gavi’, sasa ni mchezaji...

BiasharaMichezo

SBL yazindua Serengeti Oktoba Festival

Spread the love  KAMPUNI ya Bia ya Serengeti Breweries Ltd (SBL) kupitia...

error: Content is protected !!