Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia afungua maonyesho ya nanenane, atoa maagizo nchi nzima
Habari za Siasa

Samia afungua maonyesho ya nanenane, atoa maagizo nchi nzima

Makamu wa Rais Samia Suluhu, akizindua Jengo la Kituo cha Elimu kwa Wakulima Kanda ya Ziwa Mashariki Uzinduzi wa Sikukuu ya Wakulima Nanenane leo katika Viwanja vya Nyakabindi Simiyu
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania, imeagiza wizara, taasisi za umma na binafsi kutumia maonesho ya kilimo ‘Nanenane’ kama jukwaa la wakutanisha wadau wake, kwa ajili ya kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazowakabili. Anaripoti Mwandishi Wetu, Simiyu … (endelea).

Agizo hilo limetolewa leo Jumamosi tarehe 1 Agosti 2020 na Mama Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais wakati anafungua maonesho ya Nanenane mkoani Simiyu na yatahitimishwa tarehe 8 Agosti 2020.

Mama Samia amezitaka wizara pamoja na taasisi hizo, kuwekea mkazo wa changamoto za ukosefu wa masoko, mifumo ya upatikanaji mitaji, maeneo ya uwekezaji pamoja na miundombinu ya usafirishaji, uchukuzi na uhifadhi.

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, akizindua Muongozo wa Kitaifa wa Uongezaji wa Virutubisho katika matumizi ya mazao ya Chakula

“Kila wizara, taasisi za umma na binafsi ziwe mstari wa mbele kuwakutanisha wadau wa sekta husika, kujadili changamoto zilizopo,”amesema.

“Suala la masoko, miundombinu ya usafirishaji, uchukuzi na na uhifadhi iwe kipaumbele katika majadiliano yenu, suala hili lifanye katika maonesha kote nchi,” amesema Mama Samia.

Mama Samia amesema, Serikali ya awamu ya tano imefanya kazi kubwa katika kuongeza mnyororo wa uzalishaji na thamani ya bidhaa za kilimo kupitia Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015.

“Nyote ni mashahidi wa kazi zilizofanywa na awamu ya tano ikiwa ni pamoja na kusimama na wakulima katika mnyororo mzima wa uzalishaji na uongezaji thamani bidhaa za kilimo. Kupitia Ilani ya CCM mwaka 2015/20 tumetekeleza ahadi tulizotoa kwa wakulima,” amesema Mama Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!