Sunday , 3 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Samia afungua maonyesho ya nanenane, atoa maagizo nchi nzima
Habari za Siasa

Samia afungua maonyesho ya nanenane, atoa maagizo nchi nzima

Makamu wa Rais Samia Suluhu, akizindua Jengo la Kituo cha Elimu kwa Wakulima Kanda ya Ziwa Mashariki Uzinduzi wa Sikukuu ya Wakulima Nanenane leo katika Viwanja vya Nyakabindi Simiyu
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania, imeagiza wizara, taasisi za umma na binafsi kutumia maonesho ya kilimo ‘Nanenane’ kama jukwaa la wakutanisha wadau wake, kwa ajili ya kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazowakabili. Anaripoti Mwandishi Wetu, Simiyu … (endelea).

Agizo hilo limetolewa leo Jumamosi tarehe 1 Agosti 2020 na Mama Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais wakati anafungua maonesho ya Nanenane mkoani Simiyu na yatahitimishwa tarehe 8 Agosti 2020.

Mama Samia amezitaka wizara pamoja na taasisi hizo, kuwekea mkazo wa changamoto za ukosefu wa masoko, mifumo ya upatikanaji mitaji, maeneo ya uwekezaji pamoja na miundombinu ya usafirishaji, uchukuzi na uhifadhi.

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, akizindua Muongozo wa Kitaifa wa Uongezaji wa Virutubisho katika matumizi ya mazao ya Chakula

“Kila wizara, taasisi za umma na binafsi ziwe mstari wa mbele kuwakutanisha wadau wa sekta husika, kujadili changamoto zilizopo,”amesema.

“Suala la masoko, miundombinu ya usafirishaji, uchukuzi na na uhifadhi iwe kipaumbele katika majadiliano yenu, suala hili lifanye katika maonesha kote nchi,” amesema Mama Samia.

Mama Samia amesema, Serikali ya awamu ya tano imefanya kazi kubwa katika kuongeza mnyororo wa uzalishaji na thamani ya bidhaa za kilimo kupitia Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015.

“Nyote ni mashahidi wa kazi zilizofanywa na awamu ya tano ikiwa ni pamoja na kusimama na wakulima katika mnyororo mzima wa uzalishaji na uongezaji thamani bidhaa za kilimo. Kupitia Ilani ya CCM mwaka 2015/20 tumetekeleza ahadi tulizotoa kwa wakulima,” amesema Mama Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko aagiza wakurugenzi TANESCO kukemea rushwa kwenye maeneo yao

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Uongozi wa Samia kuendelea hadi 2030

Spread the loveKWETU sisi tuliowahi kusoma sekondari, iwe O levo au A...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Bado askari wastaafu wanaonewa

Spread the loveRAIS wangu Samia Suluhu Hassan tunaendelea kumshukuru Mungu kwamba wote...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Tunastawisha ufisadi na kuchukia matunda yake

Spread the loveBUNGE la Jamhuri linaloendelea mjini Dodoma, kwa wiki nzima limetawaliwa...

error: Content is protected !!