Tuesday , 21 March 2023
Home Kitengo Michezo Samatta: Nawashukuru Aston Villa, nimetimiza ndoto zangu
Michezo

Samatta: Nawashukuru Aston Villa, nimetimiza ndoto zangu

Spread the love

NAHODHA wa timu ya soka ya Tanzania ‘Taifa stars’ Mbwana Samatta ameishukuru timu ya Aston Villa kwa kumwezesha kutimiza ndoto zake za kucheza LIgi Kuu ya Uingereza (EPL). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Samatta aliyejiunga na Aston Villa Januari 2020 kwa mkataba wa miaka minne na nusu akitokea KRC Genk ya Ubelgiji, leo Ijumaa tarehe 25 Septemba 2020 ametangazwa na timu ya Fenerbahce ya Uturuki kuwa mchezaji wake mpya.

Tayari Samatta ameanza mazoezi na timu yake mpya inayoshiriki Ligi Kuu ya Uturuki.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Samatta akiwa Aston Villa alicheza michezo 16 na kufunga magoli mawili, amewashukuru timu nzima na mashabiki kwa ushirikiano waliompa.

“Naishuruku Aston Villa kwa kunipa nafasi ya kufikia ndoto zangu za kucheza Ligi Kuu ya Uingereza.”

“Shukrani za kipekee ziwafikie mashabiki wote wa Aston Villa kwa ushirikiano walionipa katika kipindi chote nikiwa na Villa. Nawatakia kila la kheri,” amesema Samatta

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!