Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Sam Misago, Charles, Rwenyagira wamfuata Zembwela Wasafi Radio
Habari Mchanganyiko

Sam Misago, Charles, Rwenyagira wamfuata Zembwela Wasafi Radio

Spread the love

KITUO cha Radio cha Wasafi kimezidi kuibomoa East Afrika Radio baada ya kuwang’oa watangazaji wengine watatu ambao wamejiunga na radio yao hivi karibuni. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Ikiwa ni wiki mbili baada ya kituo hicho kumuondoa Mtangazaji nguli wa East Afrika TV na Radio, Hilary Daudi ‘Zembwela,’ nyota wengine , Charles William, mtangazi wa kipindi cha East Africa Breakfast, David Rwenyagira wa East Africa Drive na Sam Misago wa E News na Friday Night Live (FNL).

Charles ambaye alipotea hewani ghafla katika kipindi hicho, ameliambia MwanaHALISI Online kuwa; “Nimeachana na East Africa Radio tangu 24 Oktoba, 2019 baada ya kufanya nao kazi tangu Julai, 2018. Naushukuru uongozi wa kituo hicho na wafanyakazi wote kwa ushirikiano waliompatia.”

Charles amesema kuhusu kipindi gani atakachokua akitangaza kitawekwa hadharani mara baada ya taratibu za kiofisi zitakapokamilika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!