Thursday , 18 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Sakata la Moto K/koo: Chadema wataka Majaliwa, Simbachawene wajiuzulu
Habari za SiasaTangulizi

Sakata la Moto K/koo: Chadema wataka Majaliwa, Simbachawene wajiuzulu

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua soko la Kariakoo lililoungua moto jana jioni
Spread the love

 

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),  Kanda ya Pwani, kimemtaka Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, ajiuzulu kwa kushindwa kudhibiti maafa katika tukio la moto uliounguza Soko Kuu la Kariakoo, jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Wengine waliotakiwa kujiuzulu kufuatia sakata hilo ni , Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene na  Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini, John Masunga.

Wito huo umetolewa leo Jumanne, tarehe 13 Julai 2021, mkoani Dar es Salaam na Kaimu Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani, Baraka Mwago, baada ya kutembelea soko hilo, jana tarehe 12 Julai mwaka huu.

Moto huo ulianza kuwaka usiku wa Jumamosi, tarehe 10 Julai 2021. Serikali imeunda tume ya kuchunguza chanzo cha moto huo, ambayo inatarajia kutoa taarifa yake Jumapili tarehe 18 Julai mwaka huu.

Mwago amesema kuwa, viongozi hao wanapaswa kuwajibika kutokana na kushindwa kusimamia vyema taasisi zilizo chini yao, zinazoshuhulikia masuala ya majanga nchini.

“Kamishna Jenerali wa zimamoto,  waziri wa mambo ya ndani hata waziri mkuu wanapaswa kujiuzulu. Sababu katika ofisi ya waziri mkuu   kuna kitengo cha maafa lakini kila siku taarifa zile zile, mzee wangu Kasim Majaliwa apishe labda aletwe mwingine ambaye ataweza kusimamia kitengo hicho,” amesema Mwago.

Mwago ameongeza “kuna sababu gani hawa watu kuwa ofisini? Lazima tutengeneze utaratibu watu kuwajibika. Kama hili linafanyika katika soko kuu lakini wanaendelea na nafasi zao. Tunawasihi  waone sababu ya kuona aibu. Tuombe mtupishe na muondoke.”

Mwanasiasa huyo amesema kuwa, Simbachawene alitakiwa kujua utendaji wa jeshi la zimamoto, badala ya kuuliza maswali juu ya changamoto za jeshi hilo, ambayo yalipaswa kuulizwa na wananchi.

“Waziri Simbachawene anatoa maneno ya kukinzana, yeye ndiye anayesimamia kikosi cha kuzima moto anatuhoji. Hili jambo ilitakiwa tuulize sisi ambao hatuna mamlaka hayo. Na bado anaendelea kuwa ofisini na wala hajashtuka,” amesema Mwago.

Jana, Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Temeke, Bakari Mrisho, alitaja changamoto zilizosababisha  jeshi hilo kuchelewa kuuzima moto huo,  ikiwemo mabomba ya maji ya kuzimia moto (Fire Hydrants), kushindwa kufanya kazi kutokana na kuwa na kasi ndogo ya utoaji maji.

Changamoto nyingine iliyokwamisha zoezi hilo, ni baadhi ya wananchi wasiokuwa waaminifu kwenda katika eneo la tukio kwa ajili ya kufanya uhalifu.

Pamoja na changamoto ya mrundikano wa bidhaa za wafanyabiashara barabarani, hali iliyochelewesha magari ya zimamoto kupita.

4 Comments

  • Hakika suluhu ya maswala ya Majanga hapa Kwetu Tanzania imekosekana kiasi kwamba imekua utamaduni wa kila siku kusingizia na majibu mepesi.

    Alilolisema Mwanasiasa Mwango, naliunga mkono viongozi hawa yaani Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Ndani ( Kassim Majaliwa Kassimu and Simbachawene) wapishe ofisini kuruhusu uchunguzi. Na ili kuleta ufanisi wa ofisi hizo ili kurejesha imani kwa Umma.

    Kwa sababu sio wakati wa Waziri wa mambo ya Ndani kwanza kuelezea au kuuliza changamoto za Jeshi la Uokozi na zimamoto baada ya Majanga kama haya kutokea, badala yake ilikua ni busara kwao kufuatilia na kusimamia utaratibu ikiwa ni pamoja na kukagua mara kwa mara hizo water hydrants hata wakati ambao hakuna majanga kuliko kufika wakati kumetokea majanga kama hivi waongelee habari za kwamba maji yalikua hayatoki kwa kasi.

    Uwajibikaji ni jambo la msingi.

    WAPISHE OFISINI.

  • Habari imekuwa ya kisiasa zaidi. Mwenye soko hajatajwa kuhusika. City Council inayomiliki soko na hizo fire hydrants ndio wa kwanza walaumiwe

  • Tusiendeleze zama za moronic. Kila nyumba 10,000 zimamoto mbili na ambulesi moja.
    Pesa za viwanja na majengo ziende huko theluthi moja.
    Mipangomiji warudishe maeneo ya watoto na zimamoto!

  • Tusiendeleze zama za moronic. Kila nyumba 10,000 zimamoto mbili na ambulesi moja.
    Pesa za viwanja na majengo ziende huko theluthi moja…tuache ujinga.
    Mipangomiji warudishe maeneo ya watoto na zimamoto!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia atua Uturuki kwa ziara ya siku 5

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumatano amewasili nchini Uturuki kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia arejesha mikopo ya 10%, bilioni 227.96 zatengwa

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amerejesha utaratibu wa utoaji mikopo...

Habari za Siasa

Rais Samia amfariji mjane wa Musa Abdulrahman

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumanne amempa pole Mwanakheri Mussa...

error: Content is protected !!