Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa SAKATA LA MEYA UBUNGO: Tamisemi yaingilia kati 
Habari za Siasa

SAKATA LA MEYA UBUNGO: Tamisemi yaingilia kati 

Spread the love

HATMA ya Meya wa Ubungo, Boniface Jacob, sasa iko mikononi mwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

“Tayari mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo, Betrice Dominic, tayari amemaliza wajibu wake. Hawezi kubadilisha maamuzi ya kile alichokitenda.  Ninachosikitika ni kwamba mpaka sasa, hatuna barua ya Jacob badala yake tunasikia matamko kutoka kwa John Mnyika,” ameeleza Naibu Waziri wa nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Mwita Waitara.

Akizungumza nje ya ukumbi wa Bunge, mjini Dodoma, leo Jumatatu, Waitara alisema, tayari TAMISEMI ilishapokea barua kutoka kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo, kutujulisha kuuhusu kuondolewa kwa meya huyo.

Waitara amesema, “mjadala wowote kuhusu nafasi ya meya wa ubungo haipaswi kuwa katika mazungumzo tena kwani Tamisemi inatambua hakuna meya Ubungo.”

Ameingeza: “Katibu mkuu wa Chadema hana mamlaka hata kidogo ya kumtaka mkurugenzi kufanya jambo lolote hivyo kutoa tamko kuhusu mkurugenzi ni kujichanganya.”

Akijibu swali ikiwa Chadema ambako yeye alihudumu hadi nafasi ya ubunge, kama katiba yake inaruhusu kata kumfukuza diwani, Waitara amesema, katiba ya chama inaruhusu hata tawi kumfukuza diwani kama anakwenda kinyume na maadili na matakwa ya chama.

Alisema Katiba ya Chadema iko wazi namna anavyoifahamu na kama haijabadirika bado iko sahihi na walioandika barua wako sahihi hakuna walipogushi.

Amemtaka Boni badala ya kuhangaika kwenye mitandao ya kijamii kwa lengo la kutafuta huruma, Waitara amesema, “ni vema akaleta rufaa kwetu au aende mahakamani.”

Jacob alitangazwa kutokuwa meya wa Manispaa ya Halmashauri ya Ubungo, juzi Jumamosi, kufuatia uongozi wa kata yake ya ubungo, kumuandikia barua mkurugenzi wa manispaa hiyo, kuwa amevuliwa uwanachama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!