Saturday , 2 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Sakata la kukamatwa Tito laibua utata, hajulikani alipo
Habari Mchanganyiko

Sakata la kukamatwa Tito laibua utata, hajulikani alipo

Spread the love

LICHA ya Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kukiri kumshikilia Tito Magoti, Ofisa Programu wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), haijulikana mahala alipo mwanaharakati huyo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Leo tarehe 21 Desemba 2019 jijini Dar es Salaam, Familia ya Tito pamoja na LHRC wamewaeleza wanahabari kwamba, hawafahamu Kituo cha Polisi anaposhikiliwa mwanaharakati huyo.

Wakili Anna Henga, Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, amesema baada ya Kamanda Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, jana kukiri kuwa wanamshikilia Tito, wametembelea vituo vyote vya polisi, lakini hawakumkuta mwanaharakati huyo.

“Mpaka tunatoa tamko hili hatujui ni kituo gani cha polisi anachoshikiliwa ndugu Tito, vituo vyote vikubwa tulivyotembelea hakuna hata kituo kimoja kilichokiri kumshikilia, hata baada ya tamko la Kamanda Mambosasa, tulikwenda kituo cha kati hatukumkuta Tito,” ameeleza Wakili Henga.

Wakili Henga ametoa wito kwa Jeshi la Polisi kueleza Tito anashikiliwa katika kituo gani cha polisi, pamoja na makosa anayotuhumiwa, ili waendelee na taratibu za kumuombea dhamana.

“Kama sehemu ya kuiondoa nchi yetu katika dosari ya kuonekana kutoheshimu haki za raia wake, tunaliomba Jeshi la Polisi kutaja kituo cha polisi kinachomshikilia Tito na kosa la jinai wanalomtuhumu nalo,” ameomba Wakili Henga.

Edward Magoti, Kaka wa Tito, akizungumza kwa niaba ya familia ya mwanaharakati huyo, wameliomba Jeshi la Polisi kueleza mahala alipo ndugu yao.

“Sisi tunaliomba Jeshi la Polisi kueleza mahali alipo ndugu yetu, sababu hatujui kituo gani anachoshikiliwa, badala yake polisi walikwenda nyumbani kwake kupekua,” amesema Edward.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

GGML waungana na Biteko kuanika mbinu za mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoTangulizi

Mwalimu jela miaka mitatu kwa rushwa

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mfawidhi, wilaya ya Igunga, mkoani Tabora imemhukumu...

Habari Mchanganyiko

Waziri Bashungwa aagiza wahandisi kujengewa uwezo

Spread the loveWAZIRI wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameiagiza Bodi ya Usajili wa...

Habari Mchanganyiko

Heche ataka mawakili vijana kuamka sakata Mpoki

Spread the loveMWENYEKITI wa Mawakili Vijana Tanzania kutoka Chama cha Mawakili wa...

error: Content is protected !!