SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa ufafanuzi juu ya kiasi cha dola za kimarekani 20, 000 (zaidi ya Tsh 43 milioni), zilizotolewa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), kwenda kwa Wallace Karia, ambaye ni Rais wa TFF. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).
TFF imeeleza katika taarifa yake kuwa pesa hizo zinazodaiwa kuwekwa katika akaunti binafsi ya Rais wa TFF, Karia, hazikuwekwa kwenye akaunti binafsi.
Jana tarehe 23 Novemba, 2020 Shirikisho la Mpira wa Miguu Dunia (FIFA) lilimfungia kwa kipindi cha miaka mitano kutojihusisha na soka Rais wa CAF, Ahmad Ahmad kwa sababu za matumizi mabaya ya ofisi na fedha ikiwemo kutoa kiasi cha dola za kimarekani 20,000 kwenda kwa TFF na Shirikisho la Mpira wa Miguu la Cap verde.
Katika taarifa yao TFF imeleeza kuwa Mei 2017, kamati tendaji ya CAF ilipitisha azimio ya kutoa kiasi cha dola za kimarekani 100,000 (zaidi ya Sh 231 milioni) kwa wanachama wake wote ambazo dola 80,000 (zaidi ya Sh 185 milioni) kwa ajili ya maendeleo ya soka na dola 20,000 kwa ajili ya Rais wa shirikisho husika kwa matumizi ya kila siku katika shughuli zao kwa kuwa hawalipwi mshahara.
Taarifa hiyo iliendelea kwa kueleza kuwa mara baada ya fedha hizo kuingia kwenye akaunti ya TFF, Rais Kalia alitoa maelekezo kuwa kiasi hicho cha dola 20, 000 kitumike katika shughuli mbalimbali ndani ya shirikisho hilo kwa kuwa kulikuwa na uwaba wa fedha.
Hii ni mara ya pili kuibuka kwa sakata hilo la matumizi hayo ya fedha kwa TFF na kulitolea ufafanuzi mara kwa mara licha ya safari hii kuiba mara baada ya kuhusishwa na kufungiwa kwa Ahmad Ahmad, licha ya TFF kueleza kuwa kamati ya maadili ya FIFA kutozungumzia chochote kuhusu fedha hizo dola 20, 000.
Mara baada ya kufungiwa kwa Ahmad Ahmad, muda mchache CAF ilmtangaza Omar Selemani ambaye ni mujumbe wa baraza kuu la FIFA kuwa Rais wa muda wa shirikisho hilo.
Leave a comment