KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wabunge na Madiwani wa chama hicho wanakutana kujadili sakata la Mwenyekiti na viongozi waandamizi wa chama hicho kukamata na kahidi kutoka na maamuzi mazito. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Lengo la mkutano huo ni kujadili mustakabali wa demokrasia nchini pamoja na kukamatwa kwa viongozi waandamizi wa chama hicho ikiwa pamoja na mipango iliyosukwa na Serikali kuhusiana kesi inayowakabiri.
Jana Mwenyekiti, Freeman Mbowe, John Mnyika, Naibu Katibu Mkuu Bara, Vincent Mashinji, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salimu Mwalimu, Mch. Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa na Ester Matiko, Mbunge wa Tarime walishtakiwa na kupelewa rumande baada ya kukosa dhamana hadi kesho hakimu atakapotoa uamuzi wa dhamana yao.
Makamo Mwenyekiti wa Chadema, Prof. Abdallah Safari amesema kesho wakitoka mahakamani kusikiliza hatma ya dhamana ya viongozi wao watakutana kujadili mustakabali wa demokrasia ndani ya nchi yao.
Prof. Safari amesema kikao hicho kitajumuisha Kamati Kuu ya Chadema, Wabunge na Madiwani na baadaye watatoa uamuzi mzito kama chama nini cha kufanya kwa kile kinachoendelea nchini kuhusasi demokrasia nchini.
“Kushikiliwa kwa viongozi wa ngazi za juu wa chama pinzani imevunja rekodi ya historia ya siasa Afrika. Sidhani katika Afrika ilishawahi kutokea tukio kama hili, ukiacha lile la mwaka 1999. Hii ni rekodi mbaya tunaiweka Tanzania,” amesema Prof. Safari.
Prof. Safari amesema wanajua malengo ya serikali kwa viongozi wao, lakini wao hawatakubaliana na mipango inayoendelea, mkutano wao utatoka na maamuzi magumu.
Kwa upande wake, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amesema kuwa kushikiliwa kwa viongozi hao wa juu kabisa wa chama chao ni makakati wa kuwafunga kama Mbunge wa mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’.
Lema amesema kuwa zipo taarifa kuwa viongozi hao kesho wanawaweza wakakosa dhamana na baadaye kesi hiyo kuendeshwa haraka haraka ili wafungwe.
Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...
By Mwandishi WetuMarch 29, 2024Spread the love TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...
By Mwandishi WetuMarch 29, 2024Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...
By Mwandishi WetuMarch 28, 2024Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...
By Mwandishi WetuMarch 28, 2024
Leave a comment