Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Sakata la kina-Mbowe, Chadema kukutana, kutoka na mazito
Habari za SiasaTangulizi

Sakata la kina-Mbowe, Chadema kukutana, kutoka na mazito

Prof. Abdallah Safari, Makamu Mwenyekiti wa Chadema (katikati) akizungumza na waandishi wa habari. Kulia Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema na Meya wa Ubungo, Boniface Jacob
Spread the love

KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wabunge na Madiwani wa chama hicho wanakutana kujadili sakata la Mwenyekiti na viongozi waandamizi wa chama hicho kukamata na kahidi kutoka na maamuzi mazito. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Lengo la mkutano huo ni kujadili mustakabali wa demokrasia nchini pamoja na kukamatwa kwa viongozi waandamizi wa chama hicho ikiwa pamoja na mipango iliyosukwa na Serikali kuhusiana kesi inayowakabiri.

Jana Mwenyekiti, Freeman Mbowe, John Mnyika, Naibu Katibu Mkuu Bara, Vincent Mashinji, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salimu Mwalimu, Mch. Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa na Ester Matiko, Mbunge wa Tarime walishtakiwa na kupelewa rumande baada ya kukosa dhamana hadi kesho hakimu atakapotoa uamuzi wa dhamana yao.

Makamo Mwenyekiti wa Chadema, Prof. Abdallah Safari amesema kesho wakitoka mahakamani kusikiliza hatma ya dhamana ya viongozi wao watakutana kujadili mustakabali wa demokrasia ndani ya nchi yao.

Prof. Safari amesema kikao hicho kitajumuisha Kamati Kuu ya Chadema, Wabunge na Madiwani na baadaye watatoa uamuzi mzito kama chama nini cha kufanya kwa kile kinachoendelea nchini kuhusasi demokrasia nchini.

“Kushikiliwa kwa viongozi wa ngazi za juu wa chama pinzani imevunja rekodi ya historia ya siasa Afrika. Sidhani katika Afrika ilishawahi kutokea tukio kama hili, ukiacha lile la mwaka 1999. Hii ni rekodi mbaya tunaiweka Tanzania,” amesema Prof. Safari.

Prof. Safari amesema wanajua malengo ya serikali kwa viongozi wao, lakini wao hawatakubaliana na mipango inayoendelea, mkutano wao utatoka na maamuzi magumu.

Kwa upande wake, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amesema kuwa kushikiliwa kwa viongozi hao wa juu kabisa wa chama chao ni makakati wa kuwafunga kama Mbunge wa mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’.

Lema amesema kuwa zipo taarifa kuwa viongozi hao kesho wanawaweza wakakosa dhamana na baadaye kesi hiyo kuendeshwa haraka haraka ili wafungwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

error: Content is protected !!