Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Sakata la kigogo Bavicha, Chadema watinga mahakama kuu
Habari Mchanganyiko

Sakata la kigogo Bavicha, Chadema watinga mahakama kuu

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimewasilisha ombi kwa mahakama kuu, masjala ya Dodoma, kuomba itoe amri kwa Jeshi la Polisi mkoani humo, kumfikisha mahakamani, Mratibu wa Uhamasishaji wa Baraza lake la Vijana (Bavicha), Twaha Mwaipaya anayeshikiliwa na Polisi tangu tarehe 30 Juni, 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, ombi hilo limewasilishwa leo Jumatatu, tarehe 4 Julai 2022, ambapo chama hicho kinaomba mahakama itoe amri Mwaipaya afikishwe mahakamani au aachwe kwa dhamana.

Mnyika amedai Mwaipaya anashikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Dodoma.

“Tayari Chadema imewasilisha habeas corpus leo mahakama kuu Dodoma, dhidi polisi kumshikilia Twaha Mwaipaya, kinyume cha sheria na kutaka apewe dhamana. Tunasubiri kupangiwa Jaji na kupewa summons. Mawakili wanaendelea na hatua nyingine,” ameandika Mnyika katika ukurasa wake wa Twitter.

Mwaipaya anashikiliwa na Jeshi la Polisi, tangu alipokamatwa Ijumaa iliyopita, akiwa mkoani Morogoro, alipokamatwa na Polisi akiwa njiani kurudi Dar es Salaam, akitokea mkoani Dodoma katika ziara ya kikazi.

Kwa mujibu wa Chadema, Mwaipaya anashikiliwa na Polisi, kwa tuhuma za makosa ya mtandaoni, anayodaiwa kufanya mkoani Dodoma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!