Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari Safari ya Chato kuwa mkoa yaanza
Habari

Safari ya Chato kuwa mkoa yaanza

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Spread the love

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema, ameitaka mamlaka ya Serikali Wilaya ya Chato mkoa wa Geita, kukamilisha haraka mchakato wa kuifanya Chato kuwa mkoa. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo Ijumaa tarehe 26 Machi 2021, katika salamu zake kwenye mazishi ya aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli.

Dk. Magufuli alifariki dunia Jumatano ya tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, Dar es Salaam na unazikwa leo Ijumaa 26 Machi 2021, nyumbani kwao Chato mkoani Geita.

Aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati Mgufuli akizindua Hospital ya Rufaa ya Chato

“Nina taarifa mchakato umeanza na ninaagiza mamlaka za chini, mkimaliza mchakato huku mtuletee tuangalie kama vigezo vimekidhi, kuwa mkoa siyo tatizo na kama vigezo havikukidhi, tutawaelekeza.”

“Na ili kumuenzi mpendwa wetu, kamilisheni tuone jinsi ya kufanya,” amesema Rais Samia

Kauli hiyo, ilikuwa anajibu maombi ya wazee wa Chato waliyoyatoa awali, kuwa enzi za uhai wake, Dk. Magufuli ambaye ni mzaliwa wa Chato, aliahidi kuifanya Chato kuwa mkoa.

Ombi hilo lilitolewa na Mzee Charles Bigambo alipokuwa akitoa salamu za wazee wa Chato.

Aliyekuwa Rais wa Tanzania, hayati Magufuli akiwa kwenye Uwanja wa ndege wa Chato enzi za uhai wake

Katika salamu zake fupi, kwenye Uwanja wa Mpira wa Magufuli akisema “leo niko Chato kwa mara ya tatu, mara ya kwanza nilikuwa Chato kwenye kampeni za mwaka 2015.”

“Mara ya pili nilikuja kumfariji kaka yetu, Dk. Magufuli kwa kuondokewa na dada yake (Minica Joseph Magufuli, mwaka 2018), na sasa nimerudi Chato, kwa dhumuni la kumuhitimisha kiongozi wetu, kaka yetu, baba yetu, mlezi wetu, mwalimu wetu kuja kumweka kwenye nyumba yake ya milele,” amesema Rais Samia

“Nilipokuja kumpa faraja, alinionyesha eneo ambalo ndugu zake wanakuwa wanasitiliwa, sikujua kama nitakuja Chato kumstili eneo ambalo alikuwa ananionyesha. Ni mambo mazito na msiba huu ni wetu sote na familia hatutawaacha,” amesema

Uwanja wa Ndege wa Chato wakati unajengwa

Rais Samia amesema “Wanachato, mpendwa wenu ameondoka, mnajiuliza itakuwaje, nataka kuwahakikishia ni kutekeleza miradi yote iliyomo kwenye ilani ya uchaguzi na zile alizotoa yeye mwenyewe na si kwa wana Chato bali ni nchi nzima.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!