Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Sabaya, wenzake wasomewa mashtaka ya uhujumu uchumi
Habari MchanganyikoTangulizi

Sabaya, wenzake wasomewa mashtaka ya uhujumu uchumi

Lengai ole Sabaya
Spread the love

 

ALIYEKUWA Mkuu waWilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya na wenzake sita, wamesomewa upya mashtaka matano katika Kesi ya Uhujumu Uchumi Na. 27/2021, inayowakabili kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha. Anaripoti Patricia Kighono, TUDARCo…(endelea).

Sabaya na wenzake walisomewa mashtaka hayo, leo Alhamisi, tarehe 9 Septemba 2021 na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Tarsila Gervas, mbele ya Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo, Patricia Kisinda.

Mbali na Sabaya, washtakiwa wengine ni, John Aweyo, Watson Mwahomange, Enock Mnkeni, Sylvester Nyegu, Nathan Msuya na Jackson Macha.

Wakili Gervas aliwasomewa washtakiwa mashtaka hayo, baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), kuipa mamlaka Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, kusikiliza kesi hiyo ya uhujumu, chini ya kifungu cha 12 (3), cha Sheria ya Uhujumu Uchumi.

Sabaya na wenzake walisomewa mashtaka hayo ikiwemo, kujihusisha na vitendo vya rushwa na kuchukua rushwa Sh. 90 milioni, kutoka kwa Francis Mrosso.

Na shtaka la kumtishia Mrosso kumfunguliwa mashtaka ya kukwepa kodi, kinyume cha sheria kwa lengo la kujipatia kiasi tajwa cha fedha.

Lingine ni matumizi mabaya ya madaraka akiwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, linalomkabili Sabaya peke yake, pamoja na shtaka la kujihusisha na kitendo cha rushwa na kuongoza genge la uhalifu yanayowakabili wote.

Sabaya na wenzake, waliyakana mashtaka hayo baada ya kusomewa, kisha Hakimu Kisinda aliiahirisha kesi hiyo hadi tarehe 13 Oktoba 2021, ambapo imepangwa kuwa siku ya hoja za awali za kesi kusomwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!