Saturday , 25 March 2023
Habari Mchanganyiko

Sabaya mafichoni

Lengai ole Sabaya
Spread the love

 

ALIYEKUWA Mkuu wa Wilaya ya Hai (DC), mkoani Kilimanjaro, Lengai ole Sabaya, yuko mafichoni, akitafakari hatma yake ya baadaye, Raia Mwema limeelezwa. Anaripoti Mwanandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Vyanzo vya taarifa kutoka kwa watu walioko karibu na Sabaya vinasema, mwanasiasa huyo amejichimbia katika hoteli moja, iliyopo maeneo ya Mbezi Beach, jijini Dar es Salaam.

Sabaya alisimamishwa kazi tarehe 13 Mei 2021 na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazimkabili.

Wakati Sabaya anatangazwa kusimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi, alikuwa mkoani Dodoma, akitokea jijini Dar es Salaam ambako alifanya mahojiano maalum na kituo kimoja cha televisheni.

“Huyu bwana yuko mafichoni pale Mbezi Beach, eneo la Afrikana, ambako amejichimbia kwa takribani wiki moja sasa,” ameeleza mtoa taarifa wa gazeti hili.

Undani wa kusimamishwa kwake, alikuwa wapi? Alirudi Hai au la, hotel aliyojificha, mabaunsa wake na mengine mengi, soma Gazeti Raia Mwema leo Jumamosi, tarehe 22 Mei 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

Habari Mchanganyiko

Uholanzi wampongeza Rais Samia kuimarisha vyombo vya habari, demokrasia

Spread the love  UBALOZI wa Uholanzi nchini Tanzania, umempongeza Rais Samia Suluhu...

error: Content is protected !!