Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Sabaya atoa hoja 10 kupinga kifungo miaka 30 jela
Habari Mchanganyiko

Sabaya atoa hoja 10 kupinga kifungo miaka 30 jela

Lengai Ole Sabaya akiwa mahakamani Arusha
Spread the love

 

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Arusha nchini Tanzania, imepokea maombi ya rufaa ya aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Hai, Mkoa wa Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya na wenzake wawili ambapo tarehe 15 Oktoba 2020 walihukumiwa kifungo cha miaka 90 jela. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mbali na Sabaya, wengine ni Silvester Nyegu (26) na Daniel Bura, kila mmoja amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia kwenye makosa matatu ya ujambazi na unyang’anyi wa kutumia silaha.

Sabaya amekata rufaa hiyo huku akiendelea na kusikiliza kesi yake nyingine inayomkabili ya uhujumu uchumi.

Katika rufaa hiyo ambayo tayari imeshapokelewa, Sabaya amewasilisha sababu zaidi ya kumi za kupinga hukumu hiyo ambayo itamuweka gerezani kwa miaka 30.

Kifungo hicho ni adhabu ya miaka 30 jela kwa kila kosa walilokutwa na hatia ambapo kila mmoja alikutwa na hatia kwenye makosa matatu tofauti ya unyang’anyi wa kutumia nguvu na unyang’anyi wa kutumia silaha.

Hata hivyo, mahakama iliamua adhabu hizo ziende kwa pamoja hivyo kila mmoja atatumia kifungo cha miaka 30 jela.

Rufaa hiyo ambayo imepokelewa mwishoni mwa wiki na kusajiliwa kwa namba 129/2021, inatokana na kesi ya jinai namba 105/2021 ambayo ilisikilizwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Odira Amworo.

Akizungumza kwa niaba ya mawakili wa waleta rufaa hao, Wakili Moses Mahuna alisema kuwa kwa sasa wanasubiri kupewa wito wa mahakama kwa ajili ya kuanza kwa shauri hilo.

Undani wa habari hii, soma Gazeti la Raia Mwema toleo la leo Jumatatu, tarehe 8 Novemba 2021, kujua sababu hizo za Sabaya kukata rufaa

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!