ALIYEKUWA Mkuu wa Wilaya ya Hai, Mkoa wa Kilimanjaro nchini Tanzania, Lengai Ole Sabaya leo Jumatano tarehe 1 Juni 2022, amepandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi mkoani Kilimanjaro na kusomewa mashtaka mengine mapya. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea).
Sabaya amepandishwa mahakamani hapo ikiwa ni siku moja imepita tangu
Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kuahirisha kusoma hukumu ya kesi nyingine ya uhujumu uchumi inayomkabili na wenzake sita.
Hukumu hiyo ilikuwa isomwe jana Jumanne tarehe 31 Mei 2022, lakini iliahirishwa baada ya Hakimu aliyekuwa anaisikiliza, Dk. Patricia Kisinda kuwa nje ya Arusha hivyo kuahirishwa hadi tarehe 10 Juni 2022.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI TV, MwanaHALISI Online na mitandao yetu ya kijamii kujua mashtaka yaliyosomwa
Leave a comment