Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Saa 72 za Magufuli Dar
Habari za Siasa

Saa 72 za Magufuli Dar

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, John Magufuli atafanya ziara ya kikazi ya siku tatu, jijini Dar es Salaam, kuanzia Jumatano hadi Ijumaa, tarehe 26 Februari 2021. Anaripoti Hamis Mguta…(endelea).

Katika ziara hiyo ya siku tatu sawa na saa 72, Rais Magufuli atazindua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyokwisha na inayoendelea.

Akizungumza kuhusu ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Aboubakar Kunenge amesema, ziara hiyo itaanza Jumatano tarehe 24 February 2021.

 

Amesema, siku hiyo saa 3:30 asubuhi, Rais Magufuli, atazindua Daraja la Juu Ubungo (Ubungo interchange) na mara baada ya hapo, atakwenda Mbezi kwaajili ya uzinduzi wa Kituo cha Mabasi yaendayo mikoani na nje ya nchi cha Mbezi Luis, saa 05:30 asubuhi.

Aidha Kunenge amesema, Alhamis, Rais Magufuli, ataweka jiwe la msingi la Ujenzi wa Soko la kisasa Kisutu, saa 03:30 asubuhi na baada ya hapo atafanya shughuli ya uzinduzi wa Jengo la Jitegemee House ambapo Kuna Studio za Channel ten na Uhuru Fm.

Kunenge amesema, siku ya Ijumaa, Rais Magufuli, atafanya shughuli ya uzinduzi wa majengo ya Chuo Cha Polisi na Kiwanda Cha kutengeneza sare za Polisi ambapo tukio hilo litafanyika saa 03:30 asubuhi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!