Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rungwe amuangukia Rais samia uhuru wa habari
Habari Mchanganyiko

Rungwe amuangukia Rais samia uhuru wa habari

Hashim Rungwe, Mwenyekiti wa Chaumma
Spread the love

 

MWENYEKITI wa Chama cha Ukombuzi wa Umma (Chauuma), Hashimu Rungwe amemshauri Rais Samia Suluhu Hassan kuzifuta sheria zote kandamizi kwa vyombo vya habari kwa kuwa sheria hizo zikwamisha uhuru wa habari. Anaripoti Faki, Dar es Salaam … (endelea).

Akizingumza na MwanaHALISI Online Rungwe leo tarehe 27 Oktoba, 2022 amesema kuwa Rais Samia anamamlaka ya kuondoa sheria hizo kwa kuwa zinakwamisha maendeleo ya nchi.

“Siku za nyuma mbona waandishi mlikuwepo mlisababisha matatizo gani?

“Mimi nafikiri Rais angeangalia hizi sheria rundo hovyo zilizowaandama waandishi kwa sababu juzi tu kulikuwa na kijana tunamtetea alikuwa anashtakiwa kwa sheria hizo. Akina Tundu Lissu nao walishtakiwa kwa sheria ya magazeti” amesema Rungwe.

Rungwe ambaye pia ni mbobevu wa masuala ya sheria amemuomba Rais Samia afanye mabadiliko yatakatoleta nafuu kwa waandishi wa habari na wanasiasa wahanga wa sheria kandamizi.

“Tunamuomba Rais Samia uwaachiwe hawa waandishi na hawa waliofungwa kwa sababu za kisiasa wawe huru nchi inawahitaji” amesema.

Rungwe amesema kukwepa kuvipa uhuru vyombo vya habari ni kuvunja katiba kwa kuwa suala hilo lipo wazi kuwa ni haki ya wananchi

“Vyombo vya habari kuwa huru ni suala la kikatiba hilo suala linaeleweka kuwa wananchi wanataka kupata habari wawelekee wananchi wenzao ili wananchi waelewe kinachoendelea nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!