Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Ronaldo, Raniel watamba tuzo za FIFA
Michezo

Ronaldo, Raniel watamba tuzo za FIFA

Washindi wa Tuzo za FIFA
Spread the love

HATIMAYE washindi katika tuzo za FIFA (The FIFA best Awards) wamefahamika jana katika hafla iliyofanyika Zurich, huku Cristiano Ronaldo akiibuka kuwa mchezaji bora wa mwaka na Claudio Raniel akichukua tuzo ya kocha bora wa mwaka, anaandika Kelvin Mwaipungu.

Ronaldo ameshinda tuzo hiyo baada ya kuwashinda Lionel Messi kutoka Fc Barcelona na Antoine Griezmann wa Atleticol Madrid, kutokana na kuwa na mafanikio makubwa katika msimu uliomalizika kwa ngazi ya klabu na timu ya taifa.

Hii itakuwa tuzo ya tatu kubwa kwa Ronaldo toka kumalizika kwa msimu 2015/16 baada ya kushinda tuzo ya Mchezaji bora wa Ulaya, Ballon d’Or na hii ya mchezaji bora wa FIFA na kuwa mchezaji mwenye mafanikio makubwa ndani na nje ya uwanja kwa mwaka 2016.

Lakini pia katika hafla hiyo kocha wa klabu ya Leicester City inayoshiriki ligi kuu nchini England Claudio Raniel alifanikiwa kutwaa tuzo ya kocha bora wa mwaka, baada ya kufanikiwa kuongoza kikosi chake kushinda ubingwa wa ligi kuu na kuifikisha timu hiyo katika hatua ya 16 bora ya ligi ya mabingwa barani Ulaya.

Raniel amewabwaga makocha Fernando Santos aliyefanikiwa kuiongoza Ureno kuchukua ubingwa wa kombe la Euro, Zinedine Zidane aliyechukua kombe la ligi ya mabingwa ulaya akiwa na Real Madrid, makocha wengine waliokuwa katika kinyang’anyiro hicho hapo awali ni Pep Guardiola, Chris Coleman, Didier Deschamps,Diego Simeone, Luis Enrique, Mauricio Pochettino na Jürgen Klopp.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!