Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa RITA yapitisha Bodi ya Wadhamini CUF Lipumba
Habari za Siasa

RITA yapitisha Bodi ya Wadhamini CUF Lipumba

Spread the love

KATIKATI ya mgogoro wa makundi mawili ndani ya Chama cha Wananchi (CUF), Wakala wa Usajili, Udhamini na Ufilisi (Rita) imesajili majina manane kuunda Bodi ya Wadhamini ya chama hicho. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Taarifa ya uundwaji wa bodi hiyo iliyopitishwa na Rita imetolewa leo tarehe 8 Machi 2019 na Magdalena Sakaya, Naibu Katibu Mkuu Bara anayetoka katika kambi ya Profesa Ibrahim Lipumba, mwenyekiti wa CUF anayeungwa mkono na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa.

Akiwa kwenye Ofisi Kuu  ya chama hicho Buguruni jijini Dar es Salaam Sakaya ambaye anatambuliwa na CUF Lipumba kama Kaimu Katibu Mkuu wa CUF amesema, bodi hiyo sasa ni halali baada ya kusajiliwa rasmi na Rita licha ya kuwepo kwa mvutano wa awali.

Hatua ya CUF Lipumba kupeleka majina na kusajiliwa Rita inatokana na uamuzi wa Mahakama Kuu uliotolewa siku 18 zilizopita wa kufuta bodi ya Lipumba iliyokuwa imesajiliwa Rita na pia kukataa majina yaliyopelekwa na Kambi ya Maalim Seif Shariff Hamad kwa madai zote hazikukidhi vigezo.

“Tuliwasilisha upya maombi kwenye ofisi ya RITA ili bodi yetu iweze kusajiliwa, kwa hiyo nafurahi kuwajulisha rasmi kwamba, nimetumiwa barua rasmi tarehe 6 mwezi huu kutoka Rita na sasa bodi yetu imesajiliwa rasmi,” amesema Sakaya.

Akizungumza na MwanahALISI ONLINE hivi karibuni, Abdul Kambaya, Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano ya Umma ya CUF Kambi ya Prof. Lipumba alisema uamuzi uliotolewa na Mahakama Kuu wa kufuta bodi ya awali ni wa kisheria na kuwa, kinachofuata kwa sasa ni kufuata utaratibu ili kuwa na bosi iliyokidhi vigezo.

“Athari yake ni kwamba, usipokua na bodi na hasa kwenye chama chenye kupata ruzuku ya serikali athari yake hamtaweza kupata ruzuku ya serikali.

“Ni kwa sababu sheria inahitaji bodi ya wadhamini ya chama kwa kuwa hao ndio wamiliki wa akaunti ya chama ambapo ruzuku ndio hupitishwa hapo,” amesema Kambaya.

Hata hivyo, hivi karibuni CUF Maalim nayo ilieleza kupeleka majina ya wajumbe ili kuunda Bodi ya Wadhamini ya chama hicho ambapo mpaka sasa haijaelezwa nini kinaendelea.

Tazama video kamili hapo chini

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

Habari za Siasa

Ushindi wa mpinzani Senegal wakoleza moto kwa wapinzani Tanzania

Spread the loveUSHINDI wa aliyekuwa mgombea  urais wa upinzani nchini Senegal, Bassirou...

error: Content is protected !!