Tuesday , 5 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Ripoti ya Polisi Kinondoni yaikaanga Chadema
Habari za Siasa

Ripoti ya Polisi Kinondoni yaikaanga Chadema

Kamanda Polisi wa Kanda ya Dar es Salaam, Jumanne Murilo
Spread the love

RIPOTI ya Jeshi la Polisi mkoa wa Kinondoni limeiweka kwenye mazingira magumu Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa kuonesha chama hicho kutoa lugha ya uchochezi katika kampeni zake za Ubunge wa Jimbo la Kinondoni. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Katika taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Jeshi hilo Mkoa wa Kinondoni, Ismail Murilo iliyotoka kwa Mkuu wa upelelezi wa mkoa huo, inaonyesha katika kampeni ya Chadema wasemaji wake wameeleza kuwa hawaogopi jeshi hilo na kwamba Chama cha Mapinduzi (CCM) kimewasababishai dhiki watanzania.

Kamanda Murilo amesema katika kampeni zilizofanyika Februari 10, mwaka huu zilikuwa zikizungumzia masuala mengi licha ya ripoti hiyo kuwasilishwa kwa eneo dogo kwenye ripoti hiyo.

Ripoti hiyo imewataja wazungumzaji ni pamoja na Joseph Kasambala, Ally Hemed, Mangweshi, Makongoro Mahanga, Boniface Jacob, Meya wa Ubungo, Halima Mdee, Mbunge wa Kawe na Easter Bulaya, Mbunge wa Bunda.

Wakati huohuo, ripoti hiyo ilieleza kuwa chama cha wananchi (CUF) kilifanya mkutano eneo la Kigogo ambapo wawaeleza wananchi kuwa wamchague mgombea wao na kwamba polisi wawe wapole. Wasemaji ni pamoja na Kilwa, Jalia Bahati, na Miraji.

Pia CCM nacho kimefanya Mkutano wake eneo la  mzimunini, wasemaji walikuwa ni Livingstone Lusinde, Mbunge wa Mtela, Joseph Msukuma, Mbunge wa Geita pamoja na Professa Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu, Hussein Bashe, Mbunge wa Nzega, pamoja na Feustine Ndungulille ambao waliwataka wananchi kumpgia kura  mgombea wao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Baba yake Ole Sabaya ashinda Uenyekiti CCM – Arusha

Spread the loveLoy Thomas Sabaya ambaye ni Baba wa aliyekuwa Mkuu wa...

Habari za Siasa

Serikali yaagiza uchunguzi chanzo maporomoko Hanang

Spread the loveSERIKALI imeagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini chanzo cha maporomoko ya...

Habari za SiasaTangulizi

Maafa Manyara: Rais Samia akatisha ziara yake Dubai

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amekatisha ziara yake...

Habari za SiasaTangulizi

Wataalaam wa miamba watua Hanang

Spread the loveWaziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na...

error: Content is protected !!