Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ripoti ya ajali ya ndege Bukoba: Vikosi vya uokoaji vilichelewa kufika
Habari MchanganyikoTangulizi

Ripoti ya ajali ya ndege Bukoba: Vikosi vya uokoaji vilichelewa kufika

Ndege ya Precision ikiwa imezama katika ziwa Victoria baada ya kushindwa kutua uwanja wa Ndege wa Bukoba, Kagera
Spread the love

TAARIFA ya awali ya ripoti ya ajali ya ndege ya shirika la Precision iliyotokea katika eneo la Ziwa Victoria Tanzania, imetolewa leo Jumanne na wizara ya ujenzi na uchukuzi nchini na kuonesha kuwa vikosi vya uokoaji vilichelewa kufika katika eneo la tukio. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma …  (endelea).

Ajali hiyo ilitokea muda wa saa 2 asubuhi saa tarehe 6 Novemba, 2022, lakini kwa mujibu wa ripoti hiyo inaeleza kuwa boti ya kitengo cha polisi wa majini, ilifika muda wa saa saba saa za Tanzania.

‘’ Boti ilifika saa saba eneo la tukio, baada ya kufika walikua na changamoto ya kuishiwa mafuta na oksijeni, kabla hawajafika, mvuvi mmoja tayari alianza kutoa maiti zilizokuwa ndani ya ndege’’ taarifa ya ripoti inasema.

Taarifa ya ripoti hiyo pia haijatoa sababu kamili ya nini kilisababisha kutokea kwa ajali, ikisema kuwa uchunguzi bado unaendelea.

Mamlaka ya usafiri wa anga Tanzania awali ilibainisha kuwa baada ya ripoti ya awali itafuatia ripoti ya uchunguzi wa awali inayotarajiwa kuchapishwa mwezi mmoja baada ya ajali na kisha ripoti kamili baada ya mwaka mmoja.

Ndege hiyo ya shirika la precision ATR 42-500 yenye namba PW 494 ilianguka kwenye ziwa Victoria mita chache kutoka uwanja wa ndege wa Bukoba, ikijiandaa kutua ikitokea jijini Dar es Salaam kupitia Mwanza.

Ajali hiyo iliua watu 19 kati ya 43 waliokuwemo akiwemo rubani na msaidizi wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

error: Content is protected !!