Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Ripoti: Floyd alikuwa na corona, Uingereza na Ujerumani zalaani
Kimataifa

Ripoti: Floyd alikuwa na corona, Uingereza na Ujerumani zalaani

Maandamano
Spread the love

UCHUNGUZI wa awali wa afya ya George Floyd umeonesha kwamba, alikuwa na maambukizi ya virusi vinavyosababisha homa kali ya mapafu corona (COVID-19). Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Ripoti iliyotolewa jana jioni Jumatano tarehe 3 Juni 2020 na Andrew Baker, Tabibu Mkuu wa Taifa imeeleza, Floyd alipimwa tarehe 3 Aprili 2020 na kubainika ameambukizwa corona.

Pia, ripoti hiyo imeeleza, mapafu ya Floyd yalikuwa na afya lakini kwenye moyo wake kulibainika kuwa na tatizo kidogo.

Na kwamba, mwili wake umekutwa na sumu kutokana na matumizi ya vinywaji ingawa inabainishwa, kuwa haiwezi kuunganishwa kwenye kifo chake.

Imeelezwa, sumu hiyo mwilini mwake inaweza kuchangia tatizo la upumuaji na mshutuko kutokana na tukio alilokutana nalo.

Pia, Boris Johnson, Waziri Mkuu wa Uingereza amesema ‘maisha ya Waafrika ni muhimu’ na kwamba, hasira walizonazo Wamarekani ndizo walizonazo watu duniani kote.

“Bila shaka, maisha ya Waafrika ni muhmimu na ninaelewa hasira inavyotawala vifua sio kwa Wamarekani pekee, bali hapa kwetu na duniani kote kutokana na tukio la polisi wa Marekani kumuua Floyd.”

“Nakubaliana na maandamano yanayofanywa kupinga mauaji hayo, lakini nukta muhimu ni kuwa maandamano lazima yafanywe kwa kufuata sheria.”

Pia, Serikali ya Ujerumani imeeleza kujifunza kutokana na kile kinachoendelea Marekani. Msemaji wa serikali hiyo Steffen Seibert, amesema, Serikali hiyo imeshtushwa na mauaji hayo yaliyofanywa na maofisa wa serikali.

“Kifo cha George Floyd, kimeshtua hapa Ujerumani na sehemu yote ya dunia. Imeshtua sana Serikali serikkali yetu ya shirikisho, kile ni kifo kilichoweza kuzuilika,” amesema Seibert.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!