SERIKALI imesema ipo mbioni kuanza utekelezaji wa ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Tabora hadi Kigoma na hatimaye kuiunganisha na nchi za Burundi, Rwanda na DRC. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tabora … (endelea).
Hayo yameelezwa leo Jumanne tarehe 12, 2022 na Mkurugenzi wa Shirika la Reli Tanzania TRC, Masanja Kadogosa wakati wa uwekaji jiwe la msingi ujenzi wa SGR kipande cha Makutupora-Tabora.
Kadogosa amesema wapo kwenye utaratibu wa kutafuta msimamizi wa mradi huo ambao baadae itaunganishwa na na kufika hadi Uvinza.
Amesema kutokea Uvinza itaunganishwa hadi Msongati Kitega-Uvira-Kindu, “na sisi tulishapata tenda ya awali ya kumpa msimamizi wa mradi.”
“Reli yetu itabeba abiria lakini biashara yetu ni mizigo na mzigo wetu ni madini ya Nikeli , Copper, Lithium, na bati ambayo ni mazito kweli kweli na usafiri unaofaa ni reli,” amesema.
Amesema reli hiyo ni ya uzito wa Excel 35 ambapo behewa moja lina uwezo wa kubeba hadi tani 120.
“Vipande hivi vilikuwa muhimu sana katika ujenzi wetu na hii ndoto ilikuwa mbali na Mh. Rais Samia Suluhu Hassan ametutimizia,” amesema.
Leave a comment