EMMANUEL Mwandemba kutoka Arusha, ndiye atakayekuwa mwamuzi wa mchezo wa watani wa jadi kati ya Simba na Yanga utakaopigwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, majira ya saa 11 jioni. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).
Mchezo huo wa Ligi Kuu utapchezwa Jumamosi tarehe 8 Mei, 2021, utasimamiwa na waamuzi wanne tofauti na mchezo uliopita ambao ulikuwa na waamuzi Sita na kumalizika kwa sare ya mabao 1-1.
Mwandemba ambaye atakuwa kati siku ya mchezo huo, alichezesha mchezo wa kwanza wa ufunguzi wa Ligi Kuu kati ya Yanga na Tanzania Prisons ambao uliisha kwa sare ya bao 1-1.
Kwenye mchezo huo, Mwandemba alitoa kadi nyekundu kwenye dakika ya 81 kwa beki wa Tanzania Prisons, Nurdin Chona baada ya kufanya madhambi.
Waamuzi wengine kwenye mchezo huo ni, Frank Komba kutoka Dar es Salaam, ambaye atakuwa msaidizi namba moja na Hamdani Saidi kutoka Mtwara, atakuwa msaidizi namba mbili huku Mwamuzi wa akiba ni Ramadhani Kayoko kutoka Dar es Salaam.
Leave a comment