Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Refa Mwandembwa apewa tena Rungu, mechi Simba na Yanga
Michezo

Refa Mwandembwa apewa tena Rungu, mechi Simba na Yanga

Spread the love

EMMANUEL Mwandembwa kutoka Arusha, ndiye atakayekuwa mwamuzi wa mchezo wa watani wa jadi kati ya Simba na Yanga utakaopigwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, majira ya saa 11 jioni. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo wa Ligi Kuu utapchezwa Jumamosi tarehe 3 Julai, 2021, utasimamiwa na waamuzi wanne tofauti na mchezo uliopita ambao ulikuwa na waamuzi Sita na kumalizika kwa sare ya mabao 1-1.

Mwandembwa anarudi kuwa mwamuzi kwenye mchezo huo, mara baada ya mchezo wa Mei 8 kuahilishwa, ambapo pia alipangwa kama mwamuzi wa kati.

Mwamuzi huyo ndiye aliyecheza mchezo wa kwanza wa ufunguzi wa Ligi, kati ya Yanga na Tanzania Prisons ambao uliisha kwa sare ya bao 1-1.

Kwenye mchezo huo, Mwandemba alitoa kadi nyekundu kwenye dakika ya 81 kwa beki wa Tanzania Prisons, Nurdin Chona baada ya kufanya madhambi.

Waamuzi wengine kwenye mchezo huo ni, Frank Komba kutoka Dar es Salaam, ambaye atakuwa msaidizi namba moja na Hamdani Saidi kutoka Mtwara, atakuwa msaidizi namba mbili huku Mwamuzi wa akiba ni Ramadhani Kayoko kutoka Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!