Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa RC mstaafu afariki dunia, CCM yamlilia
Habari za Siasa

RC mstaafu afariki dunia, CCM yamlilia

Spread the love

ALIYEWAHI kuwa mkuu wa mikoa ya Dodoma, Mara, Mtwara na Arusha kwa nyakati tofauti, Isdory Shirima amefariki dunia leo tarehe 31 Machi 2023. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi, Sophia Mjema, CCM kimepokea kwa masikitiko na huzuni taarifa ya kifo cha mkuu huyo wa mkoa mstaafu.

Mjema pia amemtaja Shirima kuwa kwa nyakati tofauti aliwahi kushika dhamana mbalimbali ndani ya CCM, ikiwa ni pamoja na Katibu Msaidizi Mkuu (CCM) – Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga.

Amesema CCM kitamkumbuka Shirima alivyokuwa mwanachama, mtumishi na Kiongozi mwaminifu, aliyetumia uwezo wake kwa maslahi mapana ya CCM na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na nchi kwa ujumla.

“CCM chini ya Uongozi wa Mwenyekiti wa Chama, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, kinatoa salaam za pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa, marafiki na wanachama wa CCM na wote walioguswa na msiba huu. Mungu ailaze roho ya marehemu mąhali pema peponi, Amina,” amesema mjema katika taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!