Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa RC Mgumba aeleza faida chuo cha uhamiaji kuwepo mkoani Tanga
Habari za Siasa

RC Mgumba aeleza faida chuo cha uhamiaji kuwepo mkoani Tanga

Mkuu wa mkoa wa Tanga, Omary Mgumba
Spread the love

 

MKUU wa mkoa wa Tanga, Omary Mgumba, amelezea faida za uwepo wa chuo cha mafunzo cha uhamiaji mkoani Tanga ikiwemo kuimarisha ulinzi na usalama wa nchi kwani eneo hilo hutumika sana kama mapito ya wahamiaji haramu. Anaripoti Urumasalu Kusung’uda, TUDARCo…(endelea).

Mgumba ameyasema hayo leo Jumatatu tarehe 15 Agosti 2022, katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi wa chuo hicho uliofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan sambamba na kufunga mafunzo ya awali ya askari wa uhamiaji kozi namba 1/2022.

Amesema eneo hilo lilikuwa likitumika kwa biashara haramu ya binadamu kwa uhamiaji haramu kwani ndiko walikokuwa yakipita majahazi kwenda sehemu mbalimbali “hivyo basi uwepo wa chuo hiki kitazuia uhamiaji haramu.”

Pia amesema ujenzi wa chuo hicho umeleta maendeleo katika mkoa wa Tanga ikiwemo kuboreshwa kwa miundombinu mbalimbali kama ujenzi wa zahanati itakayotoa huduma kwa wananchi wa mkoa huo hususani wakazi wa wilaya ya Mkinga pia uanzishwaji wa mradi mkubwa wa maji unaogharimu zaidi ya bilion 40, “haya yote ni manufaa kwa wananchi wa wilaya hii.”

Mgumba ameongezea kuwa jeshi hilo ni jipya hivyo litatoa ajira kwa wananchi ambapo kwa sasa jumla ya askari 818 wamehitimu mafunzo ya jeshi hilo.

“Watu wanapata mafunzo sio kwa maaskari wa hamiaji peke yake bali na maaskari wengine na kubadilishana mafunzo na jinsi ya kukabiliana na uhalifu kwani ni jeshi kamili na sio taasisi,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!