Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa RC Mghwira: Asanteni sana K’njaro, nao wampongeza
Habari za SiasaTangulizi

RC Mghwira: Asanteni sana K’njaro, nao wampongeza

Spread the love

 

ANNA Elisha Mghwira, aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro (RC),nchini Tanzania, amewashukuru wananchi wa mkoa huo akisema “nitawakumbuka daima.” Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea).

Ametoa shukurani hizo, leo Jumapili tarehe 16 Mei 2021, ikiwa ni siku moja imepita, tangu Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, alipoteua wakuu wa mikoa akiwemo wa Kilimanjaro, Stephen Kagaigai.

Kagaigai, aliyekuwa Katibu wa Bunge la Tanzania, anachukua nafasi ya Mama Mghwira, ambaye amestaafu. Kwa sasa ana miaka 62. Alizaliwa tarehe 23 Januari 1959, mkoani Si ngida

Katika ukurasa wake wa Facebook, Mama Mghwira ameandika “Asanteni sana Kilimanjaro.”

“Ninamshukuru Mungu kwa muda wote nilioishi na kufanya kazi Kilimanjaro. Asanteni kwa ushirikiano na mshikamano.”

“Tuendeleze umoja huu na nguvu ya pamoja kwa masilahi ya mkoa na taifa. Nitawakumbuka daima. Mungu awape kila mmoja hitaji la moyo wake,” amesema Mama Mghwira

Mama Mghwira, aliteuliwa kuwa mkuu wa mkoa huo na aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati John Pombe Magufuli, tarehe 3 Juni 2017, ikiwa ni takribani miaka miwili imepita tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa Oktoba 2015.

Katika uchaguzi huo, Mama Mghwira, alikuwa mgombea urais kupitia chama cha ACT-Wazalendo, akichuana na Hayati Magufuli na wagombea wengine. Hata hivyo, Magufuli aliibuka mshindi kwenye uchaguzi huo.

Wakati akiteuliwa kuwa mkuu wa mkoa, kuchukua nafasi iliyokuwa imeachwa wazi na Said Meck Sadiki, Mama Mghwira, alikuwa Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo.

Hayati Magufuli alipomwapisha Anna Mghwira kuwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro

Ujumbe huo wa kuwashukuru wana Kilimanajro, umepongezwa na watu mbalimbali, wakimpongeza kwa utumishi wake uliotukuta.

Shoumar B’van Mbwana amesema “niliiona nia yako nzuri kwa Watanzania tangu mwaka 2015 uliposimama kuwania kiti cha urais kwa tiketi ya ACT Wazalendo ukiwa mwanamke pekee uliyewania kiti hicho.”

“Na sasa umemaliza utumishi wako, Kilimanjaro ila bado unaweza kuendelea kufanya kitu kwa Kilimanjaro yenyewe na hata kwa Watanzania. Hongera.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!