MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam (RC), Amos Makalla amepiga marufuku ufanyaji wa biashara maeneo watembea kwa miguu hifadhi ya barabara zote za mkoa huo baada ya utaratibu huo kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani na ongezeko la ajali. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
RC Makalla ametoa maaagizo hayo leo Alhamisi, tarehe 9 Septemba 2021, alipotembelea Soko la Kariakoo na kujionea kero ya Ufanyaji biashara holela Kwenye maeneo ya watembea kwa miguu.
Kutokana na hilo, amewaelekeza mkuu wa wilaya ya Ilala kufanya kikao na wafanyabiashara hao Jumatatu tarehe 13 Septemba 2021 na kuainisha maeneo ya kuwapeleka wote waliovamia hifadhi ya Barabara.
Aidha RC Makalla amewaelekeza kuangalia utaratibu mzuri wa kufunga na kufungua baadhi ya Mitaa Kariakoo kwaajili ya kufanya biashara Kutokana na ufinyu wa maeneo ili Waweze kupata riziki.
Hata hivyo, amesema kwa tathimini aliyofanya amebaini hali ya ufanyaji biashara holela Dar es salaam ipo kwa kiwango kikubwa na kuwanyima watembea miguu haki zao za msingi.
Pamoja na hayo, RC Makalla ameelekeza manispaa zote za mkoa huo kuweka vibao vya kuzuia biashara kwenye maeneo ya watembea kwa miguu.
Kumbe hiyo ni kero. Asante kwa kutuhabarisha kuwa watembea kwa miguu wanakerwa na machinga.
Ni vyema tungekuwa na mfumo wa kitaifa wa kuwajengea mazingira mazuri machinga.
Rafiki yako,
Aliko Musa
Real estate investment consultant
Mimi nimekuwa mkaazi wa Kariakoo kwa miaka mingi na naelewa kero hii kubwa ambayo imewashinda wakuu wa serikali. Wamejaribu sana lakini hakuna linalofanyika – ni sawa na nguvu za soda. Na hili la RC Makala nalo litapita. Inasikitisha lakini serikalai kama serikali haina sera ya kitaifa kuhusu machinga, Ni RC tu anahangaika na kumuagiza DC wake. Hawa wawili watashindwa bila ushirikiano wa serikali nzima pamoja na mawaziri na hata Rais mwenywe.Km Ile machinga complex imefikia wapi? Wakubwa wamepiga mamilioni na hatumsikii mbunge Zungu akisema lolote kuhusu kero za Kariakoo
By the Way hili tatizo si la machinga peke yao. Nenda kariakoo Uhuru na utaona wenye maduka wakiweka bidhaa zao katika njia ya wapitao kwa miguu. Hawa wenye maduka pia wanachangia sana kwa kuvamia maeneo yote