Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa RC Chalamila: Nimezungumza na Rais Magufuli
Habari za SiasaTangulizi

RC Chalamila: Nimezungumza na Rais Magufuli

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya (RC), Albert Chalamika
Spread the love

 

MKUU wa Mkoa wa Mbeya (RC), Albert Chalamika amesema, Rais wa Tanzania, John Magufuli yuko salama na anaendelea na majukumu yake kama kawaida. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya … (endelea).

Leo Ijumaa tarehe 11 Machi 2021, RC Chalamila amezungumzia utekelezaji wa miradi mbalimbali mkoani huko inayotekelezwa na serikali ya awamu ya tano, huku akimpongeza Rais Magufuli kwa kuwapatia fedha za kutosha kutekeleza miradi hiyo.

“Leo asubuhi nimempigia simu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kumshukuru kwa fedha alizotupa za kutekeleza miradi ya maendeleo na kwa kweli amenijibu kwa furaha na faraja kubwa mno,” amesema RC Chalamila.

Rais John Magufuli

Katika kusisitiza hilo, Chalamila amesema “hao wanaozungumza rais yuko kwenye matibabu labda wao wako kwenye matibabu. Kwa kweli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli, he is very strong (yupo imara) na anaendelea kufanya kazi zake vizuri sana.”

RC Chalamila ametoa kauli hiyo, baada ya uwepo wa taarifa mbalimbali mitandaoni kwamba, Rais Magufuli yupo nje ya Tanzania kwa matibabu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!