Monday , 5 June 2023
Home Habari Mchanganyiko RC Chalamila aitisha maombi kumwombea Dk. Magufuli
Habari Mchanganyiko

RC Chalamila aitisha maombi kumwombea Dk. Magufuli

Albert Chalamila
Spread the love

 

MKUU huyo wa mkoa wa Mbeya amesema, maombi hayo yatafanyika kesho Ijumaa tarehe 19 Machi 2021, katika Viwanja vya Sokoine jijini Mbeya. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya … (endelea).

Chalamila amesema, ibada hiyo maalumu itahudhuriwa na viongozi wa dini wa madhehebu mbalimbali, viongozi wa kimila na taasisi za umma, wanasiasa pamoja na wananchi wa mkoa huo.

“Siku ya kesho tarehe 19 Machi 2021, Serikali ya Mkoa wa Mbeya imeandaa ibada maalumu, itajumuisha viongozi wa dini wa madhehebu mbalimbali, machifu , viongozi waandamizi wa mashirika ya umma,”amesema Chalamila.

Chalamila amesema “maombi maalumu yatafanyika katika uwanja wa Sokoine, kumuombea Rais wa Tanzania kupata mapumziko ya milele na pumziko lenye heri.”

https://www.youtube.com/watch?v=psyAWoe4kRc

Mbali na kuiombea roho ya Marehemu Rais Magufuli ipumzike kwa amani, pia maombi hayo yatalenga kuliombea Taifa katika kipindi hiki cha msiba mzito.

“Pia, yatakuwa maombi ya kuombea Taifa ili Mungu aendelee kutulinda ili sisi Watanzania tusivurugane katika kipindi chote cha maombolezo,” amesema Chalamila.

Akitangaza taarifa ya kifo hicho, Mama Samia alisema Rais Magufuli amefariki dunia katika Hospitali ya Mzena, Makumbusho, mkoani Dar es Salaam, alikokuwa anapatiwa matibabu baada ya kupata tatizo la maradhi ya mfumo wa umeme wa moyo.

Kabla ya umauti kumfika, Hayati Rais Magufuli aliiongoza Tanzania kwa muda wa miaka mitano na miezi minne, kuanzia tarehe 5 Novemba 2015 hadi 17 Machi 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

Habari Mchanganyiko

Bandari ya Kigoma kuongezewa uwezo wa kutoa huduma zake

Spread the love  SERIKALI kupitia mamlaka ya Bandari nchini (TPA), imewekeza takribani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kifo cha mwanafunzi UDOM: Tume yamsafisha naibu waziri

Spread the loveTUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini (THBUB),...

error: Content is protected !!