Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ratiba ya Msiba wa Dk. Mengi kesho, Makonda, Rungwe watoa neno
Habari Mchanganyiko

Ratiba ya Msiba wa Dk. Mengi kesho, Makonda, Rungwe watoa neno

Spread the love

RATIBA ya Msiba wa Reginald Mengi, Mkurugenzi wa Kampuni  za IPP zitafahamika kesho saa saba mchana. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Akizungumza na Waandishi wa Habari nyumbani kwa marehemu, Michael Ngalu,  Mwanasheria na Msemaji wa Familia hiyo amesema kuwa kesho saa 7 mchana familia itatoa ratiba ya mazishi ya msiba huo.

Wakati huohuo wanasiasa kadhaa walifika kwenye msiba huo na kueleza namna walivyoguswa na msiba huo.

Hashimu Rungwe, Mwenyekiti wa Chama Cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), amesema kuwa msiba wa Dk. Mengi umeligusa taifa na kwamba marehemu alikuwa rafiki wa kila mtu.

Amesema kuwa kwa upande wake hakumuona Dk. Mengi akiwa mbaguzi wa kisiasa wala dini alisaidia watu wote.

Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa  wa Dar es Salaam amesema kuwa taifa limepata pigo kufuatia msiba wa Dk. Mengi ambapo amekuwa na mchango kwa watu wengi nchini.

https://www.youtube.com/watch?v=pOGuHpTAw88

Amesema kuwa yeye na vijana wengine wengi walishikwa mkono na Dk. Mengi kwenye mchango wa kielimu na hata kifedha.

Amewatia moyo walemavu kuwa Mungu aliyemchukua Dk. Mengi atamleta mwingine atakayekamilisha lile aliloadhimia la kuwajengea kiwanda walemavu.

Abdallah Ambua, Mtangazaji wa East Afrika  Radio na Televisheni, amesema kuwa msiba huo ni mkubwa licha ya marehemu kuacha alama muhimu nchini kwa kuwafungulia milango ya fursa vijana, walemavu na wazee.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

error: Content is protected !!