RATIBA ya mazishi ya aliyekuwa Mkurugenzi Msaidizi wa Miradi ya Umoja wa Ulaya (EU), katika Wizara ya Fedha, Mhandisi Leopord Lwajabe, imelewa na familia yake. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Akizungumza na MwanaHALISI ONLINE, Mugisha Brassio, ndugu wa marehemu amesema, kesho jioni Jumatano tarehe 31 Julai 2019, mwili wa Mhandisi Lwajabe utachukuliwa kutoka chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwenda nyumbani kwake Kinyerezi, jijini Dar es Salaam.
Mugisha amesema, mwili nyumbani kwake mpaka siku ya Alhamisi tarehe 1 Agosti 2019 ambapo mwili wa Lwajabe utafanyiwa ibada fupi ya kuagwa hapo kwake nyumbani kwake.
Baada ya ibada hiyo, mwili wa Muhandisi Lwajabe utasafirishwa kwenda kijijini kwao Ihembe katika Kata ya Ihembe, Karagwe mkoani Kagera.
kwa mujibu wa Mugisha, mwili Mhandisi Lwajabe utafanyiwa ibada ya kuagwa na kisha kusikwa siku ya Jumamosi nyumbani kwao.
“Kesho jioni maiti itachukuliwa kutoka Muhimbili, inaenda kulala nyumbani kwake Kinyerezi. Alhamisi ibada fupi itafanyika nyumbani kwake na kuaga. Baadaye unasafirishwa kwenda Karagwe, Jumamosi mwili utazikwa ” amesema Mugisha.
Mwili wa Mhandisi Lwajabe ulipatikana ukiwa umening’inizwa juu ya mti, kwenye kichaka kilichopo maeneo ya Mkuranga, mkoani Pwani.
Mwili huo ulichukuliwa na kupelekwa kuhifadhiwa katika chumba cha maiti cha Hospitali ya Mkuranga, mkoani humo.
Baada ya ndugu wa marehemu Mhandisi Lwajabe kupewa taarifa, waliuchukua mwili wa ndugu yao na kuuhifadhi Muhimbili.
Kifo cha Mhandisi Lwajabe kimeacha utata hasa baada ya mazingira ya kutoweka kwake akiwa ofisini kwake tarehe 25 Julai 2019. Mpaka sasa, hakuna taarifa iliyotolewa na jeshi la polisi kuhusu chanzo cha kifo chake.
Leave a comment