BODI ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) 2020/21, imetoa ratiba ya ligi hiyo inayoshirikisha timu 18. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)
Ratiba hiyo inaonyesha, ligi hiyo itaanza tarehe 6 Septemba 2020, inatarajiwa kumalizika 15 Mei 200.
Ligi hiyo itatanguliwa na mchezo wa Ngao ya Jamii kati ya Mabingwa watetezi wa ligi kuu, Simba dhidi ya Namungo FC tarehe 29 Agosti 2020 katika dimba la Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.
Akitangaza ratiba hiyo mbele ya waandishi wa habari leo Jumatatu tarehe 17 Agosti 2020 amesema, Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Almas Kasongo amesema ligi hiyo inashirikisha timu 18 lakini mwisho wa msimu, timu nne zitashuka daraja na mbili kupanda.
Amesema, lengo ni kuhakikisha msimu wa 2021/22 utakuwa na timu 16 pekee.
Ratiba hiyo inaonyesha watani wa jadi, watakutana tarehe 18 Oktoba 2020 katika Uwanja wa Mkapa saa 11 jioni.
Ratiba yote hii hapa:-
j boy