KLABU ya Manchester United imeachana rasmi na kiungo wake Paul Pogba, mara baada ya kumaliza mkataba wake ndani ya klabu hiyo ambayo amehudumu kwa nyakati tofauti toka mwaka 2012. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)
Kiungo huyo raia wa Ufaransa mwenye taji la kombe la Dunia, anaachana na Manchester United kama mchezaji huru kufuatia kugoma kuongeza mkataba mpya siku za hivi karibuni.
Pogba ambaye amekulia kwenye klabu hiyo kwenye maisha yake ya soka, aliondoka kwa mara ya kwanza msimu wa 2012 na kujiunga na klabu ya Juventus ya Itary ambapo alihudumu kwenye msimu minne kisha 2016, alirejea tena Manchester United chini ya Jose Mourinho.
Once a Red, always a Red 🔴
Thank you for your service, @PaulPogba 👏#MUFC
— Manchester United (@ManUtd) June 1, 2022
Kurejea mchezaji huyo nadni ya Manchester United, kulimfanya kuwa mchezaji ghali wakati huyo kufuatia uhamisho wake kuwa wa bei kubwa, kiasi kilichowalazimu mashetani wekundu hao kutoa kitita cha Pauni Milioni 89.
Kwenye msimu uliomalizika Pogba amecheza jumla ya michezo 27, huku klabu yake ya Manchester United ikimaliza kwenye nafasi ya sita, na kushindwa kufuzu kucheza michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya.
I feel privileged to have played for this club. Many beautiful moments and memories but most importantly an unconditional support from the fans. Thank you @ManUtd pic.twitter.com/YLT3lUHOmT
— Paul Pogba (@paulpogba) June 1, 2022
Katika kipindi chote cha miaka sita ndani ya klabu ya Manchester United, Pogba alicheza jumla ya michezo 226 na kupachika mabao 39.
Mchezaji huyo anaondoka ndani ya Manchester United, huku ikiwa bado haijafahamaika ankwenda wapi lakini vyanzo vingi vya taarifa Barani Ulaya, vikieleza kuwa huwenda mchezaji huyo akarudi Juventus.
Leave a comment