Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Zambia aunda safu mpya ya majeshi
Kimataifa

Rais Zambia aunda safu mpya ya majeshi

Hakainde Hichilema, Rais wa Zambia
Spread the love

 

RAIS wa Zambia, Hakainde Hichilema amefanya mabadiliko ya uongozi katika vyombo vya ulinzi na usalama, siku sita baada ya kuingia madarakani, tarehe 24 Agosti 2021. Anaripoti Patricia Kighono, TUDARCo … (endelea).

Rais Hichilema ametangaza mabadiliko hayo jana Jumapili, tarehe 29 Agosti 2021, kupitia ukurasa wake wa Twitter.

“Leo jioni tumefanya mabadiliko katika vyombo vya ulinzi na usalama vya Taifa letu,” imesema taarifa ya Rais Hichilema.

Kupitia taarifa hiyo, Rais Hichilema amesema Luteni Jenerali Dennis Alibuzwi, ameteuliwa kuwa Kamanda wa Jeshi la Zambia, huku msaidizi wake akiwa ni Meja Jenerali, Geoffrey Zyeele.

Luteni Jenerali Collins Barry, ameteuliwa kuwa Kamanda wa Jeshi la Anga la Zambia (ZAF), huku naibu wake akiwa ni Meja Jenerali Oscar Nyoni.

Luteni Jenerali Patrick Solochi, ameteuliwa kuwa Kamanda wa Huduma ya Kitaifa ya Zambia (ZNS), msaidizi wake akiwa Meja Jenerali Reuben Mwewa.

Pia, Rais Hichilema amemteua Remmy Kajoba, kuwa Inspekta Jenerali wa Polisi nchini humo, huku naibu wake katika masuala ya operesheni, akiwa ni Milner Myambango, wakati Doris Chibombe, akiwa naibu upande wa utawala.

Mabadiliko hayo yamefanyika tangu Rais Hichilema aapishwe kuwa kiongozi wa Zambia, baada ya kumshinda aliyekuwa Rais wa Taifa hilo, Edgar Lungu, katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 12 Agosti 2021.

Hichilema aliyekuwa mgombea wa Chama Kikuu cha Upinzani Zambia, United Party for National Development (UPND), alishinda kiti cha urais baada ya kupata kura milioni 2.8 wakati Lungu aliyegombea kwa chama cha Patriotic Party, akishika nafasi ya pili akipata kura milioni 2.8.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

error: Content is protected !!