Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais wa Malawi amng’oa Makamu wake kwa tuhuma za ufisadi
Kimataifa

Rais wa Malawi amng’oa Makamu wake kwa tuhuma za ufisadi

Spread the love

 

RAIS wa Malawi Lazarus Chakwera amemvua makamu wake Saulos Chilima mamlama yote aliyokabidhiwa, baada ya kutajwa katika kashfa ya ufisadi iliyohusisha kandarasi za serikali. Anaripoti Rhoda Kanuti kwa msaada wa Mashirika ya Kimataifa … (endelea).

Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na Taasisi ya Kupambana na Rushwa nchini, iliwataja maafisa 53 wa sasa na wa zamani kuwa walipokea pesa kutoka kwa mfanyabiashara wa Uingereza, Zuneth Sattarkati ya mwaka 2017 mapaka 2021.

Hata hivyo makamu huyo wa rais bado hajajibu tuhuma hizo.

Hii ni kuhusiana na kandarasi 16 ambazo Huduma ya Polisi ya Malawi na Jeshi la Ulinzi la Malawi zilitoka kwa kampuni tano za Sattar, hata hivyo waliotajwa kwenye ripoti hiyo, ni pamoja na makamu war ais,mkuu wa polis ambaye amefutwa kazi.

Lakini sheria ya Malawi hairuhusu rais kumfukuza kazi au kumsimamisha kazi, makamu wake kwa vile rais huyo ni afisa aliyechaguliwa.

‘’Kitu bora ninachoweza kufanya kwa sasa, ambacho nimeamua kufanya ni kunyima ofisi yake ya majukumu yoyote, aliyokabidhiwa huku nikisubiria ofisi ithibitishe madai dhidi yake,’’rais alisema katika hotuba yake y kimataifa siku ya jumanne.

Aidha Chakwera aliungana na Chilima kumshinda Peter Mutharika, katika uchaguzi wa urais mwaka 2020, wawili hao walikuwa wameahidi kupambana na ufisadi serikalini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!