RAIS wa kwanza wa Zambia, Keneth Kaunada amefariki dunia, leo mchana Alhamisi, tarehe 17 Juni 2021. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Kaunda mwenye miaka 97, amefikwa n amauti akiwa katika moja ya hospitali nchini humo akipatiwa matibabu.
Alikuwa Rais wa Zambia kwa miaka 27 kuanzia tarehe 24 Oktoba 1964 hadi 2 Novemba 1991.
Kaunda alizaliwa tarehe 28 Aprili 1924.
Rais wa Taifa hilo, Edgar Lungu amesema, Kaunda amefikwa na mauti mchana wa leo.
Amesema, Taifa hilo limempoteza Baba wa Taifa hilo na kuwaomba familia kuwa watulivu katika kipindi hiki.
Leave a comment