EVARISTE Ndayishimiye, Rais wa Burundi amewasili mkoani Kigoma nchini Tanzania katika ziara ya kiserikali ya siku moja. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kigoma … (endelea).
Rais Ndayishimiye amewasili mkoani humo leo Jumamosi tarehe 19 Septemba 2020 asubuhi na kupokelewa na mwenyeji wake, Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli.
Kiongozi huyo wa Burundi amefanya ziara ya kwanza tangu alipochaguliwa kuwa Rais wa Taifa hilo Mei 2020.
Katika Uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma, Rais Magufuli amempokea Rais Ndayishimiye ambapo zimepigwa nyimbo za mataifa hayo mawili na ule wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na kukagua gwaride maalum.
Rais huyo wa Burundi amewasili nchini Tanzania baada ya kualikwa na Rais Magufuli.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Taifa, Profesa Palamagamba Kabudi akizungumza uwanjani hapo amempongeza Rais Ndayishimiye kwa kuchagua Tanzania kuwa nchi ya kwanza kutembelea tangu achaguliwe.
Endelea kufuatilia MwanaHalisi Online, MwanaHalisi TV na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali
Leave a comment