Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais wa Burundi atua Kigoma, JPM ampokea
Habari za Siasa

Rais wa Burundi atua Kigoma, JPM ampokea

Spread the love

EVARISTE Ndayishimiye, Rais wa Burundi amewasili mkoani Kigoma nchini Tanzania katika ziara ya kiserikali ya siku moja. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kigoma … (endelea).

Rais Ndayishimiye amewasili mkoani humo leo Jumamosi tarehe 19 Septemba 2020 asubuhi na kupokelewa na mwenyeji wake, Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli.

Kiongozi huyo wa Burundi amefanya ziara ya kwanza tangu alipochaguliwa kuwa Rais wa Taifa hilo Mei 2020.

Katika Uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma, Rais Magufuli amempokea Rais Ndayishimiye ambapo zimepigwa nyimbo za mataifa hayo mawili na ule wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na kukagua gwaride maalum.

 

Rais huyo wa Burundi amewasili nchini Tanzania baada ya kualikwa na Rais Magufuli.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Taifa, Profesa Palamagamba Kabudi akizungumza uwanjani hapo amempongeza Rais Ndayishimiye kwa kuchagua Tanzania kuwa nchi ya kwanza kutembelea tangu achaguliwe.

Endelea kufuatilia MwanaHalisi Online, MwanaHalisi TV na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

error: Content is protected !!