Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Urusi, Ukraine kukutana ana kwa ana mkutano G20
Kimataifa

Rais Urusi, Ukraine kukutana ana kwa ana mkutano G20

Spread the love

RAIS wa Urusi, Vladimir Putin na Volodymyr Zelensky wa Ukraine ambao ni mahasimu kutokana na vita inayoendelea kati ya nchi hizo mbili, wanatarajiwa kukutana ana kwa ana katika Mkutano wa nchi 20 zenye uchumi mkubwa duniani G20. Mkutano huo unatarajiwa kufanyika Novemba mwaka huu nchini Indonesia. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Katika taarifa iliyotolewa leo tarehe 30 Aprili, 2022 na Rais wa Indonesia, Joko Widodo amesisitiza kuwa Putin na Zelensky lazima wahudhurie.

Rais wa Ukraine

Rais Widodo amesema tayari ametuma mualiko kwa marais wote wawili.

Hata hivyo, kumekuwa na presha kutoka upande wa Marekani ambapo Rais Joe Biden ameshinikiza Urusi iondolewe kwenye mkutano huo.

Biden anaomba kuungwa mkono na mataifa mengine wanachama japo changamoto ya wazi ipo kwa China ambao wameshikilia msimamo wake wa kutokuunga uamuzi huo.

Aidha, Katibu wa habari wa Ikulu ya Marekani, Jane Psaki amesema: “Rais amekwishaweka wazi kwa umma mtazamo wake kuhusu Rais Putin kuhudhuria mkutano wa G20.

“Ni miezi sita kabla, hatuwezi kutabiri katika muda huu kwamba baadae itakuwaje, tumesilisha mtazamo wetu kwamba hatuoni kama anatakiwa kuwa sehemu ya mkutano huo iwe hadharani au kwa siri.”

Hata hivyo, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amethibitisha kupokea mualiko huo.

Katika taarifa yake aliyoandika kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter ameandika: “Nilikuwa na mazungumzo na Rais Jokowi, nashukuru kwa mualiko na msaada wako katika kupigania uhuru na usalama wa mipaka ya nchi.

“Lakini hasa ikiwa ni sambamba na maadhimio ya Umoja wa Mataifa, tulijadiliana masuala ya usalama na chakula, nashukuru sana kwa kunialika kwenye mkutano wa G20.”

2 Comments

  • Marekani ni nani hata amue nani aalikwe na nani asialikwe? Hiyo ni kazi ya Rais Wadodo. Biden hana auwezo huo na dunia inapaswa ikatae kuingiliwa

  • I support participation of all G20 leaders/members because politicization of trade is not in the philosophy of globalization. I cannot remember those involved in similar adventures in recent history facing similar boycotts. .However, wars cannot be used anywhere settle disagreements. We plead for peace and a quick peaceful resolution of the fighting neighbours.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!