Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Trump, mkewe waambukizwa corona 
Kimataifa

Rais Trump, mkewe waambukizwa corona 

Donald Trump, Rais wa Marekani
Spread the love

RAIS wa Marekani, Donald Trump na mkewe Melania Trump, sasa wapo karantini baada ya kukumbwa na virusi vya corona (COVID-19). Inaripoti BBC … (endelea).

Kabla ya Trump na mkewe kukutwa na corona, wasaidizi wake wawili walipimwa na kubainikwa kuambukizwa virusi hivyo.

Kupitia ukurasa wake wa twitter, Trump amethibitisha yeye na mkewe kukumbwa na virusi vya ugonjwa huo akisema ‘anajiweka karantini kwa siku 14.’

Pia Melania (50) kwenye ukurasa wake wa twitter ameandika.

Donald Trump na mkewe

”Kama ambavyo raia wengi wa Marekani wamefanya mwaka huu, Rais Trump na mimi tuko kwenye karantini nyumbani baada ya kuthibitishwa kuwa na virusi vya corona.

“Tunaendelea vizuri na nimeahirisha shughuli zote zijazo. Tafadhali hakikisha uko salama na tutashinda changamoto hii pamoja.”

Hope Hicks (31) ambaye ni mshauri wa Trump, ndio msaidizi wa kwanza wa rais kukumbwa na virusi hivyo.

Wawili hao (Trump na Hicks) walisafiri pamoja wakati Trump alipokwenda kwenye mdahalo wa Televisheni alipokabiliana na mpinzani wake Joe Biden Jumanne wiki hii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

error: Content is protected !!