Tuesday , 30 May 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Trump, mkewe waambukizwa corona 
Kimataifa

Rais Trump, mkewe waambukizwa corona 

Donald Trump, Rais wa Marekani
Spread the love

RAIS wa Marekani, Donald Trump na mkewe Melania Trump, sasa wapo karantini baada ya kukumbwa na virusi vya corona (COVID-19). Inaripoti BBC … (endelea).

Kabla ya Trump na mkewe kukutwa na corona, wasaidizi wake wawili walipimwa na kubainikwa kuambukizwa virusi hivyo.

Kupitia ukurasa wake wa twitter, Trump amethibitisha yeye na mkewe kukumbwa na virusi vya ugonjwa huo akisema ‘anajiweka karantini kwa siku 14.’

Pia Melania (50) kwenye ukurasa wake wa twitter ameandika.

Donald Trump na mkewe

”Kama ambavyo raia wengi wa Marekani wamefanya mwaka huu, Rais Trump na mimi tuko kwenye karantini nyumbani baada ya kuthibitishwa kuwa na virusi vya corona.

“Tunaendelea vizuri na nimeahirisha shughuli zote zijazo. Tafadhali hakikisha uko salama na tutashinda changamoto hii pamoja.”

Hope Hicks (31) ambaye ni mshauri wa Trump, ndio msaidizi wa kwanza wa rais kukumbwa na virusi hivyo.

Wawili hao (Trump na Hicks) walisafiri pamoja wakati Trump alipokwenda kwenye mdahalo wa Televisheni alipokabiliana na mpinzani wake Joe Biden Jumanne wiki hii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Mkutano wa Quad Hiroshima waibuka na kutafuta amani na ustawi wa Indo-Pacific

Spread the love  JITIHADA za mazungumzo ya Pande Nne (Quad), hazikuthaminiwa na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Kimataifa

Kiwango cha ukosefu wa ajira nchini China chaongezeka

Spread the love  WAKATI kiwango cha ukosefu wa ajira kwa vijana nchini...

Kimataifa

Kampuni za kigeni zahofia kuendelea na biashara China

Spread the love OPERESHENI ya kiuchunguzi inayofanywa na Serikali ya China kwa...

error: Content is protected !!