Friday , 9 June 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Trump atembeza bakuli
Kimataifa

Rais Trump atembeza bakuli

Spread the love

RAIS wa Marekani, Donald Trump ameomba ufadhili kwa ajili ya ujenzi wa ukuta ili kusaidia kuwafukuza wahamiaji kutoka nchini Mexico.

Mwezi uliopita alifuta mpango wa rais wa zamani wa Marekani Barack Obama uliofahamika kama “Dreamer” ambao ulikuwa unawalinda wahamiaji 690,000.

Hata hivyo, wanademokrat wenye ushawishi katika Bunge wamekataa mapendekezo hayo mapya.

Rais Trump aliliambia Bunge la Congress lililo na wabunge wengi kutoka chama cha Republican wengi kuwa lina miezi sita kukubaliana kuhusu sheria ya kuwasaidia Dreamers.

Hawa ni vijana ambao walipelekwa nchini Marekani kinyume cha sheria kama watoto na hivyo wanakabiliwa na hatua ya kufuzwa kutoka nchini humo.

Chini ya sera za Obama, vijana hao walikuwa na uwezo wa kuomba vibali vya kufanya kazi na kusoma, lakini wakosoaji wanasema kuwa mpango huo ni sawa na kuwapa kinga wahamiaji haramu.

Tangu mpango huo uanze kutekelekwa karibu hali ya wahamiaji 100,000 imebadilika kati ya karibu wahamiaji 690,000.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Kagame afumua tena Jeshi, awafuta kazi maofisa zaidi ya 200 wakiwemo majenerali

Spread the love  RAIS wa Rwanda, Paul Kagame, amewafuta kazi Meja Jenerali...

Kimataifa

Urusi imelipua bwawa kuu la umeme nchini Ukraine

Spread the loveSERIKALI mjini Kyiv nchini, Ukraine imeushutumu utawala wa Rais Vladimir...

Kimataifa

Rais Kagame afanyia mabadiliko makubwa jeshi, usalama wa taifa

Spread the loveRAIS wa Rwanda, Paul Kagame amefanye uteuzi wa wakuu wapya...

Kimataifa

Miili ya waliofariki kwenye ajali ya treni India, kukabidhiwa baada ya vipimo vya DNA

Spread the love  TAKRIBANI watu 260 wamefariki na wengine karibu 650 wamejeruhiwa...

error: Content is protected !!