Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Trump akubali kung’oka
Habari Mchanganyiko

Rais Trump akubali kung’oka

Donald Trump
Spread the love

DONALD Trump, Rais wa Marekani amesalimu amri mbele ya Joe Biden na sasa anajiandaa kung’oka madarakani. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Ameelekeza taasisi husika inayohusika kufanya mabadiliko ya kiuwongazi, kuanza mchakato huo kwa kushirikiana na Biden ambaye ni rais mteule wa taifa hilo.

Kwenye ukurasa wake wa twitter, Trump ameandika “haidhuru, kwa maslahi ya nchi yetu, napendekeza Emily (Emily Murphy, ofisa ofisi ya mabadiliko) na timu yake kufaya kile kinachostahili kwa kuzingatia itifaki za awali na pia nimearifu timu yangu kufanya vivyo hivyo.”

Joe Biden, Rais Mteule wa Marekani

Wafuasi wa Biden wamefurahishwa na kauli ya Trump kukubali kuondoka madarakani,”uamuzi huo ni hatua ya kiutawala ya kuanza rasmi kwa mchakato wa mabadilishano ya madaraka na mashirika husika.”

Katika uchaguzi huo uliofanyika mapema mwezi huu, Biden alitangazwa kupata kura 306 huku Trump alipata kura 232 hata hivyo, awali Trump aligomea matokeo hayo akidai, ameibiwa kura.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!