Tuesday , 3 October 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Shein ataja matukio yaliyotikisa utawala wake
Habari za Siasa

Rais Shein ataja matukio yaliyotikisa utawala wake

Aliyekuwa rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein
Spread the love

DAKTARI Ali Shein, Rais wa Awamu ya Saba wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), ametaja misukosuko aliyokumbana nayo katika utawala wake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

Mwaka huu Rais Shein anamaliza muda wake wa vipindi viwili kuiongoza Zanzibar (2010/2015 na 2015/2020), tangu alipoingia madarakani mwezi Novemba 2010.

Akihutubia wakati anavunja shughuli za Baraza la Tisa la Wawakilishi la Zanzibar, leo Jumamosi tarehe 20 Juni 2020, Rais Shein amesema utawala wake uliongoza kwa kuwa upandikizwaji chuki, dharau na uhasama.

Rais Shein amesema katika vipindi vyote viwili vya utawala wake, walikuwepo baadhi ya wananchi waliopandikiza  chuki kwa wenzao, ili kuvunja umoja na kuvuruga amani ya Zanziba.

“Vipindi vyote viwili walikuwepo baadhi ya wananchi wenzetu waliopandikiza chuki ili kuleta fadhaha na  vurugu miongoni mwa watu wamoja wanaopendana, walionesha dharau na kejeli kwa Serikali ili wananchi waichukie, waibeze na waione si serikali yao,” amesema Rais Shein.

Akieleza zaidi juu ya mikasa aliyokumbana nayo, Rais Shein amesema kuna watu waliandaa njama na hila,  ili kuleta mtafaruku.

Hata hivyo, Rais Shein amesema  njama hizo hazikufanikiwa kwa kuwa Mungu aliilinda amani ya Zanzibar.

“Ziliandaliwa njama na hila ili zitokee mtafaruku, lakini kwa uwezo wa mungu ametujalia hali ya amani, umoja, mshikamano na utulivu hadi leo kwa viwango vilevile tulivyokuwa tunatarajia. Tuwe makini na tahadhari kubwa dhidi ya wenye nia mbaya ya serikali yetu, “ amesema Rais Shein.

Rais Shein amesema anamshukuru Mungu kwa kuwa, ametekeleza ahadi yake ya kulinda amani, usalama na utulivu wa Zanzibar, licha ya changamoto alizokumbana nazo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bilioni 6.1 kumaliza tatizo la maji Katoro-Buseresere – Geita

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa Umoja wa wanawake CCM, (UWT), Zainab Shomari...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali kupokea ndege ya 14 ya ATCL, safari kuongezeka

Spread the love  SERIKALI ya Tanzania, kesho tarehe 3 Oktoba 2023, inatarajia...

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

error: Content is protected !!