Monday , 29 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Shein afanya uteuzi wa Majaji, watendaji
Habari za Siasa

Rais Shein afanya uteuzi wa Majaji, watendaji

Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein
Spread the love

RAIS wa Zanzibar, Ali Mohamed Shein amewateua Khamis Ramadhan Abdalla na Aziza Iddi Suweid kuwa majaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar, anaandika Hamis Mguta.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwenye tovuti ya Ikulu ya Zanzibar uteuzi huo umeanza jana na umefanyika kwa mamlaka aliyopewa chini ya kifungu cha 94(2) cha Katiba ya Zanzibar ya 1984.

Aidha, kwa mujibu wa uwezo wake chini ya Sheria ya Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma Namba 4 ya 2015, kama ilivyorekebishwa na Sheria Namba 4 ya 2017, Kifungu cha 10(a)(1), amemteua, Kubingwa Mashaka Simba kuwa Katibu wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Katika uteuzi mwingine, Shein chini ya kifungu cha 6(2) cha Sheria ya Shirika la Bandari Namba 1 ya 1997, amemteua Kapteni Juma Haji Juma kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bandari.

Rais Shein pia amemteua George Joseph Kazi kuwa Naibu Katibu Mkuu katika Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora anayeshughulikia masuala ya Katiba na Sheria.

Viongozi wa hao walioteuliwa wanatarajiwa kuapishwa Ikulu ya Zanzibar Oktoba 2, mwaka huu .

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

Habari za Siasa

ACT Wazalendo yaanika madudu miradi ya ujenzi, moundombinu

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi juu ya uelekeo wa...

Habari za Siasa

Samia ashuhudia utiaji saini ujenzi wa minara 758 ya bilioni 265

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa kampuni za...

error: Content is protected !!