Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Shein afanya uteuzi wa Majaji, watendaji
Habari za Siasa

Rais Shein afanya uteuzi wa Majaji, watendaji

Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein
Spread the love

RAIS wa Zanzibar, Ali Mohamed Shein amewateua Khamis Ramadhan Abdalla na Aziza Iddi Suweid kuwa majaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar, anaandika Hamis Mguta.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwenye tovuti ya Ikulu ya Zanzibar uteuzi huo umeanza jana na umefanyika kwa mamlaka aliyopewa chini ya kifungu cha 94(2) cha Katiba ya Zanzibar ya 1984.

Aidha, kwa mujibu wa uwezo wake chini ya Sheria ya Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma Namba 4 ya 2015, kama ilivyorekebishwa na Sheria Namba 4 ya 2017, Kifungu cha 10(a)(1), amemteua, Kubingwa Mashaka Simba kuwa Katibu wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Katika uteuzi mwingine, Shein chini ya kifungu cha 6(2) cha Sheria ya Shirika la Bandari Namba 1 ya 1997, amemteua Kapteni Juma Haji Juma kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bandari.

Rais Shein pia amemteua George Joseph Kazi kuwa Naibu Katibu Mkuu katika Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora anayeshughulikia masuala ya Katiba na Sheria.

Viongozi wa hao walioteuliwa wanatarajiwa kuapishwa Ikulu ya Zanzibar Oktoba 2, mwaka huu .

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chadema: Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!