Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia: Watanzania wengi hawafahamu makucha ya wakoloni
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia: Watanzania wengi hawafahamu makucha ya wakoloni

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema Watanzania wengi hawayajui makucha ya wakoloni kwa kuwa walizaliwa baada ya uhuru wa Tanzania Bara tarehe 9 Desemba 1961, hivyo hawakushuhudia madhila ya ukoloni. Anaripoti Regina Mkonde, Dar ea Salaam … (endelea).

Kiongozi huyo ametoa kauli hiyo leo Jumatano, tarehe 8 Desemba 2021, akihutubia Taifa kuelekea maadhimisho ya miaka 60 ya uhuru, kesho Alhamisi.

Kilele cha maadhimisho hayo, yatafanyika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa viongozi mbalimbali akiwemo Rais Samia na mgeni wake, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya.

Rais Samia amesema, kati ya Watanzania milioni 59 waliopo leo, ni Watanzania 2,520, 559, sawa na asilimia 4.3, walizaliwa kabla ya ukoloni.

“Takwimu hizi zinatuambia jambo jingine muhimu nalo ni kuwa Watanzania  wengi walioko leo si tu hawakuwepo wakati wa uhuru bali pia na hawayakuishi  madhila ya ukoloni wala matokeo yake.”

“Hivyo kwa kukosa kwao uzoefu wa hali ya huko nyuma, tulipotokea uwawia vigumu kutambua sababu za kujitoa katika makucha ya ukoloni na kujua thamani  ya uhuru wetu,” amesema.

“Hatua kubwa tuliyopiga na  mafanikio tuliyoyapa na tunayo yafaidi leo. Ni kwa sababu hiyo basi nikaona umuhimu wa kuhutubia taifa ili tukumbushane mawili matatu juu ya siku hii adhimu,” amesema Rais Samia.

Rais Samia amewaomba Watanzania waendelee kudumisha uhuru wao, pamoja na kulinda amani na utulivu wa nchi.

Tanzania Bara ilipata uhuru wake tarehe 9 Desemba 1961, kutoka kwa ukoloni wa Waingereza, ambapo uhuru huo ulipatikana kutokana na harakati za Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na wenzake 16, akiwemo Abdul Sykes, Ally Sykes, Joseph Kaserabantu, John Rupia, Lameck Makaranga, Abdul Kandoro na Japhety Kiriro

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!