Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia: Wanaoguswa ripoti ya CAG wanachukuliwa hatua
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia: Wanaoguswa ripoti ya CAG wanachukuliwa hatua

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) nchini Tanzania, Charles Kichere
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake inawachukulia hatua watu wanaotajwa kufanya ubadhirifu katika ripoti za ukaguzi za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza katika mahojiano yake na Kituo cha Televisheni cha Azam, yaliyorushwa leo Jumatano, tarehe 4 Mei 2022, Rais Samia amesema, Serikali huwa inafanyika kazi mapendekezo ya ripoti ya CAG, lakini haitangazi hadharani ndiyo maana wananchi hawajui hatua zinazochukuliwa.

“Kinachotokea ni kwamba, CAG anavyomalizia ripoti yake anatakiwa kuikabidhi kwa Rais, na Rais haraka anatakiwa kuikabidhi bungeni na ikifika bungeni inajadiliwa. Kawaida hoja za CAG akishakuletea serikalini, Serikali inakaa na kupitia hoja baada ya hoja. Zinazotolewa nyingi zina majibu,” amesema Rais Samia.

Rais Samia amesema “kwa hiyo tunapojibu hatujibu kwenye kamera, tunajibishana baina ya sisi na CAG, tunamwambia hili tumeshalifanyia kazi, anakuja kutizama ni ukweli anaweka tiki.”

Mkuu huyo wa nchi amesema, Serikali ilifanyia kazi ripoti ya CAG ya 2019/2020, kwa kuwachukulia hatua wahusika, ikiwemo baadhi ya watumishi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), waliotajwa kuhusika katika ubadhirifu.

2 Comments

  • Kwanini serikali “haitangazi hadharani” ? Inaogopa nini? Wezi, wabadhirifu na wala rushwa wanachukuliwa hatua bila wananchi kujua? Wananchi hawahusiki? Du hii ni ya mwaka. Mama tuambie ukweli yakhe tafadhali

  • Asante wezi wa Mali ya umma inatakiwa wanaoubiwa waelewe hatua gani walizo chukiliwa wezi hao sasa ukiwa wanchukuliwa hatua za siri walio ibiiwa ni umma wa kiitanzania usijue kweli haki haki io alioibiwa asijue hukumu ya mwizi wake

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

Habari za Siasa

CCM yakemea ufisadi, yaipa kibarua TAKUKURU

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekemea vitendo vya ubadhirifu wa...

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

error: Content is protected !!