Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia: Wabunge acheni ubabe migodini
Habari za Siasa

Rais Samia: Wabunge acheni ubabe migodini

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS Samia amewaonya wabunge kuacha kufanya ubabe katika maeneo ya migodi ili wapewe pesa na kuzitumbua badala yake wasimamie pesa hizo za hisani zitumike kwa maendeleo ya Taifa na wananchi kwa ujumla. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Pia amewaasa wawekezaji katika miradi ya uchimbaji wa madini kuzingatia kwamba suala la kurejesha fadhila kwa wananchi sio la hiyari.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 13 Disemba, 2021 katika hafla ya utiaji saini mikataba baina ya serikali na kampuni za uchimbaji madini iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Amesisitiza mali hiyo imeumbwa pale walipo hivyo ni mali yao wao na serikali.

“Kama tunakwenda kuichukua, kuichimba, kuitengeneza… lazima turudishe fadhila kwao wafaidike na kile Mungu alichowaumbia, sio tuende kuchota tuondoke, tuwaache walivyo. Kwa suala la fadhila halina hiyari,” amesema.

Pia amewaomba waakuu wa wilaya, wabunge wa maeneo husika na serikali za mitaa kutoa ushirikiano mzuri katika utekelezaji wa miradi hiyo.

“Sio kwenda kufanya ubabe migodini, kuchukua fedha ya hisani kwa wananchi na ikatumika kwa mambo mengine.

“Wabunge ambao maeneo yenu miradi hii ipo, miradi inakuja kwenu iwasaidie kujenga maendeleo ya nchi si kujijenga ninyi binafsi… kuna ile kwenda na kuwatisha wenye migodi huko kwamba kama si mimi ninyi msingekuwa hapo. Hapana!!

Amesema iwapo faida ya miradi hiyo ikirudi kwa wananchi ni alama ya kipekee kwa mbunge husika kwamba amehusika kuwa sehemu ya ujio wa mradi huo.

Aidha, ameongeza kuwa moto wa madini ulianza kuwashwa na Rais Dk. John Magufuli na yeye atauendeleza na hautazimika ili wananchi wanufaike.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

error: Content is protected !!